By
danielmjema.blogspot.com
 |
Picha ya Marehemu Meja Jenerali, Muhiddin Mfaume Kimario (76), aliyefariki dunia Oktoba 6, mwaka huu, katika Hospitali ya Apollo India alipokuwa amelazwa kwa muda mrefu akipatiwa matibabu, aliyezikwa Jana, Oktoba 11, mwaka huu katika makaburi ya Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro. |
 |
Mkuu wa Majeshi mstaafu, Meja Jenerali, Hagai Mrisho Sarakikya, akitia saini katika kitabu cha Rambirambi, Nyumbani kwa Marehemu, Meja Jenerali Muhiddin Kimario. |
 |
Mjumbe wa Halmashauri kuu wa CCM Taifa, Aggrey Mareale, akitia saini katika Kitabu cha Kumbukumbu. |
 |
Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka (kushoto) akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Moshi mjini, Elizabeth Minde msibani hapo. |
 |
Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka (kushoto, akijadili jambo na mkuu wa Majeshi mstaafu, Meja Jenerali Mrisho Sarakikya. |
 |
Mkuu wa Majeshi mstaafu, Meja Jenerali Mrisho Sarakikya, akitia saini katika kitabu cha Rambirambi. |
 |
Mkuu wa wilaya ya Rombo, Elinasi Pallangyo (aliyeinama) akiteta jambo na Mkuu wa Majeshi mstaafu, Meja Jenerali Mrisho Sarakikya. |
 |
Sheikh Salim Mubaraka kutoka Arusha akiongoza waumini na waombolezaji kusoma Talakini nyumbani kwa Marehemu Meja Jenerali Muhiddin Kimario. |
 |
Jeneza la Marehemu Meja Jenerali Kimario. |
 |
Wasanii wa Bongo Movie, Mzee Chilo (kulia) na Mzee Masinde nao walikuwepo. |
 |
Sehemu ya Waombolezaji. |
 |
Maofisa wa juu wa Jeshi la wananchi, akiwemo Meja Jenerali Ezekeil Kyunga (wa kwanza kushoto) na Mkuu wa majeshi mstaafu, Meja Jenerali, Mrisakikya (wa pili kushoto), wakifuatilia taratibu katika mazishi ya Meja Jenerali mstaafu, Muhiddin Kimario. |
 |
Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka, akitia saini katika kitabu cha Rambirambi. |
 |
Heshima za kijeshi zilifuata |
 |
Msafara kuelekea msikiti wa Riadha kwa ajili ya kuuswali mwili wa Meja Jenerali Kimario |
 |
Umati mkubwa uliojitokeza katika msiba huo. |
 |
Jeshi la Wananchi ukifanya gwaride tayari kwa heshima za mwisho. |
 |
Mwili wa Marehemu Meja Jenerali Mstaafu, Muhiddin Kimario ukiwasili katika eneo la makaburi. |
 |
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika makaburi ya Manispaa ya Moshi, kushuhudia maziko ya Meja Jenerali Kimario, kulia kwake ni Mkuu wa majeshi Mstaafu, Meja Jenerali Mrisho Sarakikya na Kaimu Mkuuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Ibrahim Msengi, kushoto kwake ni mkuu wa kikosi cha Batalion kanda ya Kaskazini, Meja Jenerali, Ezekiel Kyunga. |
 |
Ndugu wakijiandaa kuuhifadhi mwili wa Marehemu, Meja Jenerali Muhiddin Kimario. |
 |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka mchanga kaburi la Marehemu Meja Jenerali Mstaafu, Muhiddin Kimario aliyefariki, Oktoba 6, mwaka huu na kuzikwa jana katika makaburi ya manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro. |
|
|
|
0 MAOINI :