MADEREVA MOSHI WAGOMEA USHURU WA MAEGESHO
Posted in
No comments
Wednesday, June 20, 2012
By
danielmjema.blogspot.com
MADEREVA wa daladala za mjini moshi zimegoma kuingiza magari
yao barabarani kwa madai kwamba ushuru wanaotozwa kama malipo ya stika za
manispaa pamoja na ushuru ya maegesho kuwa ni kubwa mno.
Madereva hao walifikia uamuzi huo ikiwa ni wiki moja baada
ya wenzao wanaofanya usafiri katika barabara ya pasua kugoma kupakia abiria kwa
malalamiko kama hayo lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa maslahi yao na malalamiko
yao yanasikilizwa na kufanyiwa kazi.
Wakiongea na gazeti hili mapema leo madereva hao walisema
kuwa wamelazimika kugoma ili kuishinikiza halmashauri ya manispaa ya moshi
kuangalia upya ushuru wanazozitoza ambapo katika tangazo lililotolewa na
manispaa hiyo lilionesha ongezeko la ushuru kuanzia tarehe 1 julai mwaka huu.
Walisema ongezeko hilo ambalo linaonesha kuwa kila gari
litatakiwa kulipa ushuru wa shilingi 1500 kutoka katika ule wa sasa wa shilingi
1000 pamoja na malipo ya stika ya manispaa ya shilingi 10,000 kwa mwaka ni
uonevu kwani ushuru huo ni mkubwa sana na haiendani kabisa hali halisi ya
maisha.
Katika ongezeko hilo pia wapo madereva wa teksi ambao watatakiwea
kulipa ushuru wa shilingi 500 kutoka katika shilingi 200 wanayolipa sasa na
madereva wa magari makubwa ambao watalazimika kulipa ushuru wa shilingi 2000.
Akizungumza baada ya
kukutana na uongozi wa manispaa ya moshi chini ya mheshimiwa mstahiki meya wa
moshi, mwenyekiti wa usalama barabarani mkoa wa Kilimanjaro, Christopher Lyimo,
alisema kimsingi wamekubaliana na mstahiki meya kusitisha mgomo hadi tarehe 25
mwezi huu huku akianisha maklubaliano yaliofikiwa na pande zote mbili kuwa ni
pamoja na kusitisha utekelezaji wa ushuru mpya uliotangazwa.
Makubaliano mengine yaliofikiwa ni kusitisha mgomo huo,
kufuta malipo ya stika, na kuongeza kiujumla kuna malalamiko mengine 11 ambayo
manispaa imeafiki kuyafanyia kazi na kusisitiza kwamba kama mkutano wa tarehe
25 hautatoa ufumbuzi wa malamiko ya basi hawatakuwa na budi zaidi ya kuendelea
na mgomo wao.
“tumekubaliana kusitisha mgomo, kufuta ushuru huu ambao
hatuelewi mantiki yake, tumekubaliana kwa pamoja kwamba malipo ya stika ya
manispaa pia isitishwe, tutasitisha mgomo hadi tarehe 25, siku ambayo
tutakutana tena na manispaa isipokuwa kama maswali yetu hayatapatiwa ufumbuzi
katika kikao hicho basi mgomo utakuwa palepale”, alisema Lyimo.
Kwa upande wake mkuu wa usalama wa barabarani mkoa wa Kilimanjaro,
SSP- Peter N. Sima, aliyeongea kwa niaba ya mkuu wa jeshi la polisi mkoa wa Kilimanjaro,
alisema wao kama polisi hawatakuwa tayari kuvumilia vitendo viovu vya uvunjifu
wa amani na kuwataka wananchi kutopenda kufanya vurugu inapotokea tatizo.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako

0 MAOINI :