Thursday, June 14, 2012

MADEREVA WA BODA BODA WALIVAMIA GARI


 Pichani ni gari lenye nambari T 491 ATR lililoharibiwa na madereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda,likiwa limeharibiwa vibaya kwa kuvunjwa vioo vyote Juni 9 mwaka huu,majira ya saa nne asubuhi baada ya kumgonga dereva mwenzao Mtaa wa Kabwe,Jijini Mbeya hapa kisha kutokomea.
 Lakini madereva bodaboda hao walimfukuzia mpaka Mtaa wa Mama John,Jijini humo,ambapo walimpiga baada ya kukataa kutii amri ya kulipeleka gari polisi.Hata hivyo hivi sasa Jeshi la Polisi wanawatafuta vijana wa bodaboda wanaotuhumiwa kuharibu gari hilo.

No comments:

Post a Comment