Saturday, June 23, 2012

MADIWANI WAMESEMA HAWAHUSIKI KATIKA KINACHOENDELEA KATIKA MANIISPAA YA MOSHI


MADIWANI wa chama cha mapinduzi CCM, wameema wao hawa husiki katika kile kinachoendelea katika baraza la madiwani wa manispaa ya mjini moshi kutokana na mtafaruku amba umekuwa ukifukuta katika baraza hilo katika siku za hivi karibuni.

Madiwani walisema kuwa katika baraza hili linaloundwa na madiwani wengi wa CHADEMA, kumekuwa na mapungufu megi katika uongozi na usimamiaji wa miradi ya maendeleo katika manispaa kitu ambacho kimekuwa kikisababisha mkwaruzano wa mara kwa mara kati ya wananchi na uongozi wa manispaa.

Walisema katika vipindi ambavyo baraza limeongozwa na Madfiwani wa CCM, hakujawahi kuwepo kwa malumbano kama inavyojitokeza hivi sasa.

Akiongea katika mkutano wa hadhara wa CCM, uliofanyika katika kata ya korongoni, katika manispaa ya moshi, katibu wa CCM wilaya ya Moshi, Aloo Segamba alisema, mambo yanayoendelea kwa sasa katika baraza hilo ni thibitisho tosha kwamba CHADEMA hawafai kupewa uongozi.

Segamba alisema, katika siku za hivi kumekuwa na mikwaruzano mengi baina ya wananchi na uongozi wa manispaa na kutolea mfano tukio la hivi karibuni la mgomo wa madereva wa daladala wakipinga kutozwa ushuru mkubwa wa maegesho na manispaa hiyo.

“Kinachoendelea katika baraza hili linatosha kutupa picha kamili ya aina ya uongozi ambao tungeuweka madarakani endapo tungeichagua CHADEMA kuongoza nchi hii,” alisema Segamba.

Mwenyekiti wa wazazi CCM mkoa na mjumbue wa kamati ya siasa, Thomas Ngawaiya, alisema kuwa kuichagua chadema kuongoza nchi hata kwa dakika ni dhambi ambayo kama wananchi watadiriki kuifanya katika uchaguzi wa 2015, matokeo yake yatakuja kuonekana katika kizazi kinachokuja.

“Hawa watu ni mafisadi wakubwa kuliko hata ilivyo kwa CCM wanayoinyoshea kidole kila kukicha, wanazunguka nchi nzima na viongozi wao wote wakitumia jasho la mwananchi, jamani huu si ufisadi huu, alisema Ngawaiya na kuongeza

“ tukifanya kosa la kuwapa nchi yetu watuongeza dhambi hiyo itakuja kuonekana matokeo yake katika kizazi chetu cha baadae,” alisema Ngawaiya.

No comments:

Post a Comment