Ni Uhalisia Huu Unaotutaka Tuwachukie Wanasiasa Wenye Kuendekeza ....
Posted in
No comments
Sunday, June 10, 2012
By
danielmjema.blogspot.com


....Ubaguzi
wa kisiasa. Wenye kupandikiza mbegu za chuki za kidini, kikabila na
hata kikanda miongoni mwetu Watanzania. Nimepata kuandika, kuwa Tanzania
ina vyote, kasoro Watanzania.
Kwamba
kinachokosekana ni uzalendo. Mioyo ya wanasiasa wetu wengi imejaa hila
badala ya nia za dhati za kuijenga nchi yetu. Na kama mwanasiasa ana
nia ya dhati ya kuijenga nchi yetu hawezi akawabagua Watanzania wenzake
wengine wasishiriki siasa na kuijenga nchi yao.
Ndio
maana, hata teuzi za wajumbe wa bodi za mashirika ya umma zinatokana na
itikadi za vyama; kwamba walio nje ya chama tawala wanabaguliwa, kana
kwamba hao hawawezi kuwa na michango ya kuimarisha mashirika ya umma.
Halafu tunashangaa kuwa Reli haifanyi kazi, Atcl inavurunda, bandari
kugeuka kuwa kijiwe cha wajanja wenye kutafuna, TBS kuachwa ikivurunda
mpaka Bodi nzima inakatiwa tiketi kwenda Japan kwa fedha za umma,
kujaribu kuyaficha madudu ya TBS, na mengi mengineyo.
Ndugu zangu,
Hii
ni Nchi Yetu. Ni nchi yetu sote. Haya yote yasitufanye tuichukie nchi
yetu tuliyozaliwa, bali yatutie hamasa zaidi ya kuipigania nchi yetu.
Nilifikiri
ningeandika sentesi mbili tu kuhusu picha hizo mbili. Nimejikuta
naandika mengi. Ndiyo, inasikitisha kuwaona Watanzania wenzetu hao
pichani kuwa umuhimu waokwa wanasiasa uonekana wakati wa kukaribia
kwenda kuwaomba kura. Tena, dhiki yao ndio huwa mtaji wa wanasiasa. Kwa
hila na ghilba hushawishiwa, kwa vipande vya khanga, bakuli za sukari
na hata lita za pombe ya kupima , kuwapigia kura wanasiasa. Kisha
wanatelekezwa.
Ndugu zangu,
Tuna
lazima ya kuwapigia kelele wale wote wenye kutenda maovu kwa nchi yetu.
Wenye kuwadhalilisha Watanzania wenzetu kwa sababu ya umasikini wao
uliotengengezwa na baadhi ya wanasiasa wao. Maana, pamoja na yote haya,
jahazi la nchi yetu halijazama, linayumba sana.
Siku
ile tutakapoacha kuwapigia kelele viongozi wanaoisaliti nchi
tuliyozaliwa kwa matendo yao, basi, ndio utakuwa mwanzo wa jahazi la
nchi yetu kuzama. Na historia itakuja kutuhukumu. Kwa kukaa kwetu kimya.
Na mwanakijiwe
IRINGA
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako

0 MAOINI :