OPERESHENI ZUIA UHALIFU YANASA MBAO 79 MOSHI

Posted in
No comments
Thursday, June 21, 2012 By danielmjema.blogspot.com


JESHI la polisi mkoani kilimanjaro linamshikilia mtuhumiwa mmoja mkazi wa kibosh manushi, manispaa ya moshi vijijini, wilayani kilimanjaro kwa kosa la kuvuna miti bila kibali.

Akitoa ripoti ya mafanikio ya operaesheni kuzuia uhalifu mkoani hapo mkuu wa jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro, kamanda Robert Boaz, alisema jeshi hilo kupitia kwa operesheni hiyo ijulikanayo kama operesheni zuia uhalifu, ulifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo akiwa na mbao 79.

Alisema kwamba jeshi hilo lilipata taarifa kutoka kwa raia wema na mara moja kufika nyumbni kwa mtuhumiwa huyo aliyemtaja kuwa ni Beda Mallya Mmasi, akiwa nyumbni na walipombana aliwaonesha alipoku amezihifadhi mbao.

Boaz alisema, kuwa hadi sasa hawajafanikiwa kujua thamani kamili ya mbao hizo pamoja na aina lakini wanafanya mawasiliano na iodara ya maliasili ili kuweza kujua thamani na aina ya mbao zilizokamatwa.

Operesheni zuia uhalifu mkoani Kilimanjaro ilianzishwa tarehe 8 juni mwaka huu na tayari kwa msaada wa wananchi imeshaweza kukamata  watuhumiwa 25 wakiwa na 28.5kg za mirungi, 83.5 kg za bhangi ambapo jumla ya watuhumiwa 14 walikamatwa.

Alisema kuwa tayari jeshi limekamata jumla ya watuhumiwa 14 wakiwa na lita 105 za pombe haramu aina ya gongo, watuhumiwa 2 wa unyan’ganyi wa kutumia silaha pamoja na katoni 62 pombe bandia ya konyagi aina ya viroba zenye viroba 144 ambapo watu 3 walikamatwa wakiwa na mitambo 2 ya kutengeneza pombe haramu ya moshi.


Aidha kwa upande wa makosa ya usalama barabarani, kamanda boaz alisema, jumla ya madereva 376 walikamatwa na makosa 711 ambapo katika makosa hayo tayari tozo la ‘notification’ lililolipiwa Tsh. 23,630,000.
Makosa hayo ni pamoja na mwendo kasi wa magari, ubovu wa magari, madereva kutokuwa na leseni, magari kutokuwa na leseni, kuzidisha abiria na magari kutokuwa na bima.

Mdau wetu, Moshi.


Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .