Waandamanaji wakaidi polisi Khartoum

Posted in
No comments
Sunday, June 24, 2012 By danielmjema.blogspot.com


Waandamanaji mjini Khartoum, Sudan, wametumia matairi waliyoyaasha moto na mawe kuwazuwia polisi waliojaribu kuzima maandamano dhidi ya serikali kupinga hatua ya serikali ya kubana matumizi.

Moshi wa matayri yaliyochomwa kwenye maandamano mjini Khartoum

Maandamano hayo awali yaliongozwa na wanafunzi, lakini inaarifiwa na wananchi wengine nao wamejiunga nayo.

Polisi wa Sudan wameamrishwa kuchukua hatua haraka kumaliza fujo hizo.
Maandamano hayo yaliyoanza tarehe 16 Juni, yalichochewa na hatua za serikali za kupambana na msukosuko wa kiuchumi, uliotokana na Sudan Kusini kusimamisha kusafirisha mafuta yake kwa kupitia Sudan.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .