Thursday, January 30, 2014

JESHI LA POLISI LINAMSAKA JAMBAZI SUGU TANZANIA

IGP- Ernest Mangu

Polisi Nchini Tanzania wanamsaka mtu mmoja aliyewauwa watu nane kwa kuwapiga risasi na kuwajeruhi wengine watatu.Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita, siku ya Jumamosi usiku eneo la Kaskazini mwa Mkoa wa Mara.

Kwa mujibu wa Mashuhuda wa tukio hilo, Jambazi hilo lilikuwa likitaka kupewa pesa na simu za mkononi toka kwa waathiriwa.

Kikosi maalum kinachojumuisha maafisa wa polisi wapatao 160 kimeundwa na mekabidhiwa jukumu la kumsaka jambazi huyo kwa nia ya kumtia mbaroni.

Mwanahabari wa BBC Nchini Tanzania anasema kuwa sio kawaida kwa watu wa Mara wanaopakana na Ziwa Victoria kubeba bunduki katika harakati za kulinda mifugo wao.

No comments:

Post a Comment