KENYA: SIMBA WATOROKA MBUGANI NA KUINGIA MITAANI NAIROBI
Posted in
afrika mashariki
No comments
Friday, February 19, 2016
By
danielmjema.blogspot.com

Shirika hilo limewataka wakaazi wa maeneo hayo kutahadhari. Hii si mara ya kwanza kwa wanyama hao kuzua taharuki katika eneo hilo.
Msemaji wa Shirika hilo Paul Udoto ameambia BBC nchini Kenya kwamba wamepokea habari kwamba simba hao wa kike walionekana katika nyumba za NHC katika eneo la Langata na mitaa mengine inayopakana na Barabara ya kusini.
''Haya ni maeneo ambayo yana watu wengi, na hii ndio maana tumeimarisha msako wetu,'' aliambia BBC kwa njia ya simu, yeyote aliye na habari kuwahusu anapaswa kutoa habari hizo mara moja.
Langata ni eneo lililo na watu wengi na maafisa wa KWS pamoja na polisi wanahofia kwamba wanyama hao huenda wakasababisha hasara iwapo hawatapatikana haraka na kurudishwa katika mbuga hiyo.
Simba sita waliripotiwa kutoroka katika mbuga hiyo Alhamisi jioni lakini wanne kati yao walipatikana .
Habari Zingine
- WENGI WALIVYOJITOKEZA KUMUAGA MWANA TBN JENNIFER LIVIGHA (CHINGA ONE) HOSPITALI YA AMANA JIJINI DAR
- Wachimbaji mgodi 15 waliokwama ardhini waokolewa nchini Tanzania
- Al-Shabab washambulia kambi ya majeshi ya Kenya nchini Somalia
- UHURU WA HABARI SIO KUIANGALIA TU SERIKALI - MWAKYEMBE
- JUKWAA LA WAHARIRI TANZANIA LATANGAZA KUSUSIA KUANDIKA HABARI ZA MKUU WA MKOA WA DAR
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :