Mwanamuziki wa Bongo Flava, Tunda Man leo amenusirika kifo
baada ya kupata ajali mbaya eneo la Idetelo, katikati ya Nyololo la
Makambako, nchini Tanzania
Kwa mujibu wa Tunda Man akiwa amesinzia ghafla alisikia mlio
mkubwa uliopelekea gari yao kupoteza muelekeo na kuelekea porini, ndani
ya gari yao kulikuwana watu watano ambao mmoja wao alifariki dunia papo
hapo huku wengine wakijeruhiwa.
Aidha Tunda Man amemtaja marehemu kuwa
ni Mussa maarufu kwa jina la Man Katuzo ambaye taratibu za kusafirisha
mwili wake kuupeleka Kilosa mkoni Morogoro zinaendelea.
Source: GPL

No comments:
Post a Comment