HIVI ULISIKIA ILE STORI KWAMBA WACHEZAJI WA TWIGA STARS WANASHIRIKI MAPENZI YA JINSIA MOJA? UPANDE WA PILI NDIO HUU….

Posted in
No comments
Wednesday, June 27, 2012 By danielmjema.blogspot.com

.
Vyombo mbalimbali vya habari vya Tanzania likiwemo gazeti la Mwananchi vimenukuliwa vikiripoti stori kwamba Kocha wa timu ya taifa ya Twiga Stars aliejiuzulu Boniface Mkwasa alisema moja kati ya mambo yaliyomkera Twiga Stars ni wachezaji kadhaa kushiriki katika mapenzi ya jinsia moja, wao kwa wao kwenye timu.

Exclusive on millardayo.com Nahodha wa timu hiyo Sophia Mwasikili amesema “nimefurahi kulizungumzia hilo swala kwa sababu limekua likizungumzwa kwenye magazeti mengi bila uthibitisho, kocha hakuzungumza kwamba kuna vitendo kama hivyo alisema vilikuepo kipindi cha nyumba lakini kwa sasa havipo, nimekua Twiga Stars toka 2006 mpaka sasa sijaviona hivyo vitendo labda mwalimu ndio aliona kwa mchezaji lakini hakuna yeyote ambae amewahi kuripoti kwangu”

“Wazazi wetu hawajapenda hili swala, tumedhalilishwa na hata kama kuna mchezaji alifukuzwa kutokana na hilo basi itakua ni siri kati yake na mwalimu hatujawahi kuambiwa, kama Mkwasa atapatikana ni vizuri amtaje huyo mtu il iwatanzania wajue lakini kiukweli hakuna vitendo kama hivyo Twiga Stars” – Sophia

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .