UZINDUZI WA KILIMANJARO MARATHON 2013 KATIKA UKUMBI WA MORIO MOSHI

Posted in
No comments
Saturday, December 1, 2012 By danielmjema.blogspot.com







IBRAHIMU MSENGI-DC MOSHI


INSP.LISTON NEPACHA MWENYEKITI KAA


ALLEN MARO-TPC




GEORGE KAVISHE- MENEJA KILIMANJARO PREMIUM LAGER




MSIMU wa kumi na moja wa mbio za kimataifa za Kilimanjaro Marathon zinazotarajiwa kufanyika Machi 3, mwaka 2013, umezinduliwa Rasmi hapo Jana Mjini hapa katika Ukumbi wa Morio Hall.

Akizungumza katika uzinduzi huo Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndiyo wamekuwa wadhamini wakuu wa mbio hizo tangu zilipoanzishwa mwaka 2003, George Kavishe alisema, wao kama wadhamini wakuu wamedhamiria kufanya mabadiliko makubwa katika mbio hizo na kuzifanya kuwa na hadhi ya kimataifa zaidi.

“Sisi kama wadhamini wakuu wa mbio hizi zinazoshirikisha wakimbiaji kutoka kila kona ya Dunia, tumedhamiria kuhakikisha tunaboresha mbio hizi na kuzifanya kuwa sura ya kimataifa,” alisema Kavishe

Alisema kutokana na matokeo ya mbio za mwaka huu, yaliyofanyika mapema Februari, na kushuhudia 
wakenya wakitawala mbio hizo, safari hii wamejipanga kwa kutoa changamoto ya zawadi zaidi ya kawaida kwa mshindi wa kwanza kutoka Tanzania ambapo kwa mshindi wa kwanza, wanaume na wanawake kutoka Tanzania atapata Shilingi milioni sita ikiwa ni mara mbili zaidi ya zawadi za kawaida.

“Tumeboresha mashindano nah ii ni kitu kipya , kwani kutokan ana aibu ya mashindano ya mwaka huu, mwaka ujao kila mshindi wa kwanza kutoka ndani ya nchi atapata maara mbili ya fedha za mshindi wa kwanza,” alisema Kavishe.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa wilaya ya Moshi, Dkt.Ibrahimu Msengi, aliwataka wanariadha wote watakaoshiriki kuhakikisha kuwa kile kilichotokea katika mashindano ya liyopita hasa ya mwaka huu yanbaki kuwa sehemu ya Historia.
Alisema Mkoa umefurahishwa sana kuwepo kwa mashindano hayo mkoani hapa na antarajia mbio hizo zitachangia katika kukuza sekta ya Utalii, Uchumi na mahusiano ya kimataifa kutokana na kushirikisha wakimbiaji kutoka mataifa mbalimbali kutoka katika kila kona ya dunia.

Wakati huohuo Mwenyekiti wa chama cha Riadha mkoani Kilimanjaro (KAA), Liston Nepacha alibainisha kuwa kwa kushirikiana na chama cha Riadha Taifa (RT), wamedhamiria kufuta mapungufu yote yaliyojitokeza katika mbio za mwaka huu na kuongeza kuwa tayari ya kikosi cha Tanzania kinaendelea na Maandalizi katika Kambi yaop iliyoko Holili, Himo mkoani Hapa.

Mashindano ya Kilimanjaro Marathon yanayofanyika kila Mwaka yanadhaminiwa na Kilimanjaro premium Lager, Kilimanjaro Drinking Water, Arusha Hotel, Gapco wanaodhamini mbio za watu wenye Ulemavu, Bonite, Kiss Hotel, TPC, Shoprite, KK security, Simba Cement, Merenga Investment, CFAO Motors na yanatarajia kuwa na washiriki wapatao 6000.


Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .