SEMI FINAL UEFA: MAN CITY VS REAL MADRID HAKUNA MBABE
Posted in
Michezo
No comments
Wednesday, April 27, 2016
By
danielmjema.blogspot.com


Huu ni mchezo ambao takwimu zilikuwa zinaibeba Real Madrid kwa kiasi kikubwa kulikoMan City ambao walikuwa nyumbani, 24 July 2015 Man City akiwa nyumbani alifungwa goli 4-1 na 21 Nov 2012 alitoa sare ya goli 1-1 katika uwanja huo wa Etihad, takwimu ambazo hazioneshi dalili nzuri akicheza na Real Madrid katika uwanja huo.

Licha ya kuwa mchezo umemalizika kwa sare ya 0-0, Real Madrid kwa mujibu wa takwimu walikuwa wanatajwa kuwa na safu imara ya ushambuliaji kuliko Man City , kwaniReal katika mechi zake tano zilizopita hivi karibuni walikuwa wamefunga jumla ya magoli 18 na kufungwa matatu, wakati Man City walikuwa wamefunga magoli 11 na kufungwa mawili.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :