Lowassa Aongoza Harambee Kuchangia Mpango Wa Elimu Kata Ya Kipawa Jijini Dar Es Salaam

Posted in
No comments
Friday, June 8, 2012 By danielmjema.blogspot.com


















WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, ameendelea kuwa mstari wa mbele katika harakati zake za kuchangisha mamilioni ya fedha baada ya kuchangisha Sh. 421,850,000 kwa ajili ya kuboresha Mfuko wa Elimu Kata ya Kipawa katika Manispaa ya Ilala, jijini Dar es Salaam.
Lowassa, ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), aliendesha harambee hiyo juzi katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Kempiski Jijini Dar es Salaam ambapo yeye mwenyewe alichangia Sh. milioni 10.

Katika harambee hiyo miongoni mwa kampuni yaliyochangia kiasi kikubwa ni Lions Club Sh. milioni 70, Home Shopping Center Sh. milioni 22, African Barrick Gold Dola 10,000, Songas Dola 10,000, Maersk Sea Line ilichangia Sh. milioni 90, na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja alichangia Milioni Sh.10.

Wengine waliochangia ni madiwani, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, Chadema, taasisi za watu binafsi na mtu mmoja mmoja ambapo Radio Clauds walitoa muda wa hewani wa kutangaza mpango huo wenye thamani ya Sh. milioni 12.
Akizungumza kabla ya kuendesha harambee ya kuchangisha, aliwataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea kuwahamasisha wananchi kuwekeza katika kuchangia Sekta ya Elimu. 
CHANZO:KIJIWE BLOG

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .