WANACHAMA wa chama cha mapinduzi CCM, tawi la longoi kijiji
cha Longoi nguzo nne kata ya Machame weruweru wameulalamikia uongozi wa CCM katikia
tawi hilo kwa kuuza eneo la chama kwa taasisi ya mradi wa maji sadi na salama
wa mkalama bila ridha ya yao.
Tuhuma hizo, za matumizi mabaya ya mali ya chama
zimeelekezwa kwa mwenyekiti wa CCM tawi la Longoi, Francis Shiyo, zikimlaumu
kutoa eneo la chama kwa taasisi ya mradi wa maji bila ya ridhaa ya wanachama.
Wakiongea na MTANZANIA katika nyakati tofauti mwenyekiti wa
jumuiya ya wazazi CCM kata ya Machame weruweru, Raphael Munishi na Mjumbe wa mkutano
mkuu CCM tawi la longoi, Lothi Pyuza walisema kuwa pamoja na kamati ya siasa ya
chama kupinga utoaji wa eneo hilo
alikataaa kukubaliana na maamuzi ya kamati.
Munishi alisema hapo awali, waliomba kupewa eneo hilo ili wajenge ofisi ya chama wakanyimwa lakini cha
kushangaza jamaa hawa walipokuja eneo hilo
lilitolewa haraka na kuongeza kwamba kilichowashangaza zaidi ni utaratibu
uliotumika katika kuidhinisha eneo hilo
kuchukuliwa.
Akizungumzia tuhuma hizo, mwenyekiti wa CCM Tawi la longoi,
alikana tuhuma hizo na kusema kwamba mradi wa mkalama unaohusisha vijiji vitano
vya mkalama, kawaya, Longoi, kikavu na mjengweni ulijenga ofisi zake hapo baada
ya wanachama wote na kamati ya siasa kuridhia eneo hilo kupewa kwa mradi kutokana na kijiji cha
longoi kuwa katikati hivyo kuwa kiunganishi cha vijiji vyote.
Meneja wa mradi wa mkalama, Godwin Iddo, alisema anashangaa
kuona watu wanaingiza siasa katika miradi ya maendeleo kama hiyo na kusisitiza
kwamba uwepo kwa ofisi hiyo katika eneo hilo kihalali na kuongeza kwamba ili kuthibitisha
kuwa mradi uko hapo kihalali mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Hai
akiongozana na mhandisi mkuu wa wilaya alifika na kubariki ujenzi wa ofisi hiyo.
Iddo alisema katika uzinduzi wa ofisi hiyo, uliofanyika
tarehe 25 mei mwaka huu, mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama,
aliyewakilishwa na mkuu wa wilaya ya Hai wakati huo, Norman Sigalla alisema
ujenzi wa ofisi na kazi za mradi wa maji katika kijiji hicho ni moja katika
utekelezaji wa sera za CCM kwa hiyo inashangaza kusikia mradi huo unawekewa
pingamizi.
Hata hivyo katika mkutano uliofanyika hapo jana na
kuongozwa na katibu wa chama cha mapinduzi wilaya ya Hai, Hassani Mtega,
kilitoa hadi tarehe 28 juni mwaka huu kwa viongozi wa mradi wawe wameshaondoka
katika eneo husika au wafanye utaratibu wa kukutana na uongozi wa CCM tawi la
longoi ili kuangalia uwezekano wa kupata eneo lingine la kujengea ofisi yao.
MWISHO
No comments:
Post a Comment