WANANCHI WAIGOMEA UONGOZI UJENZI WA BARABARA
Posted in
No comments
Monday, June 18, 2012
By
danielmjema.blogspot.com
WANANCHI wa kijiji cha Okaseni, kata ya Uru Kusini, wilaya
ya Moshi vijijini, mkoani Kilimanjaro, wameiomba serikali kuwahimiza viongozi wao katika ngazi za kata
na taarafa kuchunguza miradi inayoanzishwa katika vijiji vyao ili kuhakikisha
inaendelea ili kuepuka hasara kwa taifa na kuleta manufaa kwa watanzania wote.
Wakizungumza na KIJIWE BLOG katika nyakati tofauti, wananchi
hao walilalamikia miradi mingi inayoanzishwa katika vijiji vingi kuishia njiani
huku hela na nguvu za wananchi zikiteketea kutokana na uzembe na ufatiliaji
mbovu miongoni mwa viongozi na waendeshaji wa miradi.
Wakitolea mfano barabara ya kuanzia kwa eno shop iliyoko katika
kata ya Uru kusini hadi katika ofisi ya kijiji cha Okaseni nakusema, awali
ilitumia shillingi million 24 fedha zilizotolewa na mfuko wa maendeleo wa
jamii, TASAF, ili kutengeneza barabara hiyo, ujenzi ulioanza mwaka 2007 lakini
cha kushangaza mpaka sasa mradi huo haujakamilika jambo ambalo limezidi vichwa
vyao huku maswali yao yakikosa majibu.
Hali kadhalika, mwaka 2011, chama cha msingi cha KNCU, kilitoa
Tsh Milioni 2, kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo ambapo katika maelezo ni
kwamba hele hizo zingetumika kujengea eneo la eno shop hadi ofisi ya kijiji.
Aidha walisema kuwa ili kuonesha kuwa kulikuwa na ubadhirifu
wa fedha za umma, ujenzi wa barabara hiyo ilikuwa inafanyika nyakati za usiku
ambapo walmkuta mkandarasi aliyepewa dhamana ya kujenga barabara ya kwa eno
shop akiendelea na shughuli za ujenzi majira ya saa tatu usiku na wakiwa
kaitika harakati za kuhoji ni kwa nini kazi hiyo ifanyike usiku alikuja
mwenyekiti wa kitongoji hicho ambaye walimtuhumu kufuja fedha za mradi huo.
Wakijibu tuhuma hizo, uongozi wa kijiji cha okaseni, walikiri
kuwepo kwa mradi huo na kusema kwamba shilingi milioni 2 zipo kwenye akaunti ya
kijiji na kudai kwamba walimuomba mkandarasi huyo kusaidia kufukia makorongo
yaliyopo katika baadhi ya mabarabara ya kijiji kwa gharama zao na kusisitiza
kuwa hamna hela ya mradi iliyotumika mpaka sasa.
“Ni kweli kama wanavyosema wananchi barabara ililimwa majira
ya jioni, hilo kwa kweli sibishi lakini kitu nisichokubaliana nacho ni kudai
kwamba hela zimetumika, nataka niweke wazi kwamba eneo hilo nilimwomba yule mkandarasi
anisaidie kufukia makorongo yale tena kwa gharama zangu mwenyewe wakati
mikakati ya kujenga barabara ikiendelea,” alisema mwenyekiti wa kitongoji cha okaseni
kati, Alphonce Mtaresi, ambaye kipande cha barabara kilicholimwa kipo
kitongojini kwake.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya Uru kusini, Joseph Komu,
alisema hana taarifa ya fedha za mradi wa TASAF wa mwaka 2007 kwani katika
kipindi hicho hakuwa madarakani na kuongeza kuwa shilingi milioni 2 za KNCU
alizipokea na kukabidhi kwa uongozi wa kijiji ila baada ya kupata tetesi kwamba
barabara inajengwa usiku aliandika barua kwa uongozi wa kijiji na kuwapa siku 7
kuanzia tarehe 12 juni hadi 19 juni
mwaka huu wawe wamempa taarifa kamili za mkandarasi huyo na mahali fedha
zinazotumika katika ujenzi huo zinapopatikana.
na mwandishi wetu, moshi
na mwandishi wetu, moshi
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako

0 MAOINI :