Friday, March 1, 2013

MAANDALIZI YA KILIMANJARO MARATHON YAMEKAMILIKA; MJI WA MOSHI UKO TAYARI....!!!

KILI MARATHON INATARAJIWA KUFANYIKA MACHI 3, 3013 KATIKA MANISPAA YA MOSHI MKOANI KILIMANJARO MAANDALZI TAYARI.

Maandalizi ya mbio za kimataifa ya Kilimanjaro marathon yanayotarajiwa kufanyika kesho yameshakamilika, aambapo kamera ya TAIFA LETU.com ilipita maeneo mbali mbali na kukuta kila kitu kikiwa sawa tayari kwa mbio hizi zinazosemekana kuwa za kipekee.

Mbio za Kilimabnjaro Marathon 2013 zinatarajiwa kufanyika katika uwanja wa chuo cha ushirika Msohi ambao mpaka sasa tunapozungumza umeshaandaliwa kwa kazi ya kupokea wageni.

wakati huohuo, Waziri wa Michezo, Habari na Utamaduni Dkt. Fenella Mkangala anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika mbio hizo zitakazoanza kutimua vumbi majira ya saa 12;00 asubuhi kwa mujibu wa waandaaji na waratibu Kampuni ya Executive Solutions.
 

No comments:

Post a Comment