LOWASSA AMFAGILIA JK MAREKANI
Posted in
No comments
Friday, July 19, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
Na Swahili TV
Alisema kitendo cha Rais wa Marekani Mhe. Barack Obama, kuja nchini na viongozi mbalimbali wa mataifa makubwa kumeonyesha Rais Kikwete anakubalika.
“Ni hivi karibuni tu Rais Xi Jinping wa China, Rais Obama na Rais mstaafu wa Marekani George W.Bush walikuwa nchini Tanzania, hii inaonyesha kuwa Tanzania iko juu katika medani za kimataifa” alisema Mheshimiwa Lowassa.
Mheshimiwa Lowassa ambaye yuko nchini Marekani kwa ziara ya kikazi,
aliongeza kwa kusema, Rais Kikwete anastahili pongezi sana kwa hilo
kwani sio rahisi kwa viongozi wa mataifa makubwa kutembelea nchi
zingine labda kama mko juu sana katika medani za kimataifa.
Pia
alisema Rais Kikwete amekuwa akihusishwa na utatuzi au ushauri wa
kutatua matatizo mbalimbali ya nchi zingine na pia ameanza kuishirikisha
Tanzania katika usimamizi wa amani katika nchi mbalimbali.
Tanzania
iliweka historia hivi karibuni kwa maraisi wawili wa Marekani kukutana
katika nchi moja kwa wakati mmoja, Rais Barack Obama na George W.Bush
walikutana jijini Dar es Salaam mwezi huu.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :