MTWARA KIMENUKA TENA!!!
Posted in
No comments
Friday, July 19, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
HALI
ya mambo imeanza kuwa mbaya baada ya kuenea kwa habari kuwa baadhi ya
wananchi wa mjini Mtwara waliivamia gari lililobeba mabomba ya gesi
kutoka mjini humo.
Gari hilo lilikuwa limebaba mabomba hayo kutoka
Mjini Mtwara kuelekea jijini Dar es Salaamlimeshambuliwa na mawe na kupelekea dereva wa lori
hilo kujeruhiwa vibaya na kuibua taharuki.
Lori hilo lilianza kushambuliwa mara baada ya
kuingia katika Manispaa ya Mikinda Mtwara Mjini sababu ya kushambulia gari hilo
ni katika kile kinacho dhihirisha kuwa wanamtwara bado
hawajakubaliana na hoja ya Serikali ya kutaka kusafirisha gesi hiyo kwa ajili
ya manufaa ya nchi.
Lori hilo kwa sasa lipo kituo kikubwa cha polisi Mtwara, ikiwa
ni wiki moja tu imepita tokea watu kadhaa kukamatwa na jeshi la polisi mkoani Mtwara kwa kile kinachodaiwa kusambaza waraka wa kuhujumu miundombinuu yote ya gesi mara tu serikali itakapo anza utekelezaji wake wa ujenzi wa bomba hilo kupeleka jijini Dar es Salaam kama ilivyokubaliwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :