PRESHA YATISHIA UHAI WA JACKLINE WOLPER
Posted in
No comments
Friday, July 19, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
STAA wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper ameeleza kuwa, tatizo alilonalo
la presha ya kushuka huenda siku moja likawa chanzo cha kifo chake kwani
linapomjia, huwa katika hali mbaya sana.
Akizungumza hivi karibuni Wolper alisema, tatizo hilo amekuwa nalo kwa
muda mrefu na kufikia hatua ya kwenda kutibiwa nchini Afrika Kusini
likapungua lakini sasa limerejea na linamkosesha amani.
“Kwa kweli hili tatizo la presha ya kushuka nililonalo ipo siku litaniondoa duniani, unajua wakati mwingine hali hiyo ikinijia natokwa na damu nyingi puani, huoni ni tatizo kubwa hili!” alisema Wolper.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :