SUPER D AINGIZA MKANDA WA NGUMI SOKONI
Posted in
No comments
Sunday, July 21, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
Super D aachia DVD mpya za mapigano kuendeleza mchezo wa masumbwi
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KOCHA wa mchezo wa masumbwi hapa nchini, Rajabu Mhamila
‘Super D’, amesema kuwa kitendo cha kutengeneza DVD za ngumi ni hatua yake ya
kuhakikisha kuwa vijana wanajifunza masumbwi.
Kazi za Super D zilizoingia sokoni.
Alisema anaamini kuwa wengi wanaobahatika kuona CD hizo wana
uwezo wa kupata mwangaza na mahitaji ya kujikita zaidi katika mchezo wa
masumbwi na hatimae kufikia malengo yao waliyojiwekea.
Alisema kitendo cha bondia chipukizi kuwa na muda wa kukaa
na kujifunza ngumi kwa kuangalia waliyompita kiwango ni jambo lenye kutia moyo
katika harakati za mchezo wa masumbwi duniani.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :