BULEMBO: "VIBOKO KATIKA SHULE ZA JUMUIYA YA WAZAZI CCM NI LAZIMA"
Posted in
No comments
Sunday, July 21, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
Na Mwandishi Wetu, Hai
Mwenyekiti wa Jumuiya ya
wazazi ya chama cha mapinduzi (CCM) na mjumbe wa halmashauri kuu ya Taifa, Abdallah
Bulembo ameagiza kuendeleza adhabu ya viboko kwa wanafunzi wote wanaosoma
katika shule zinazomilikiwa na jumuiya ya wazazi kote nchini ili
kurudisha nidhamu mashuleni.
Bulembo aliyasema hayo jana wakati
akiongea na walimu na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Wari iliyoko katika
wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, na kusema kuwa suala la viboko katika shule
za wazazi ni lazima.
Alisema malezi kwa vijana hivi
sasa yameporomoko kutokana na wazazi kutowajibika ipasavyo hali ambayo
imemesababisha vijana wengi kutowaheshimu walimu, na hata wakati mwingine mzazi
amekuwa akidiriki kumwadhibu mwalimu eti kisa kampiga mtoto wake.
“Suala la viboko kwa wanafunzi
wanaosoma katika shule za wazazi lazima ili kumweka katika malezi mazuri maana
hata sisi tulichapwa viboko ndiyo maana leo hii mnapotuona hapa ni kutokana na
malezi tuliyolelewa na wazazi wetu na ndio maana tumefika hapa tulipo hivi
sasa”alisema Bulembo.
Alisena sisi wazazi tumnasema
huwezi kuendelea kuwalea wanafunzi kama ambavyo wazazi wao wanavyotaka, na kama
mzazi anaona kuwa mwanae hawezi kuchapwa viboko amwondoe hapa.
Aidha bulembo aliongeza kwa kusema
kuwa wapo baadhi ya wanafunzi hawalipi ada na akatoa agizo kwa wanafunzi
wote ambao hawajalipa karo ya shule kuondoka katika maeneo ya shule hizo ili
kutafuta shule ambazo zinapokea wanafunzi wasiokuwa na ada.
“Katika hili nitakuwa mkali kweli
mwanafunzi, asiyelipa ada aanze kufungasha mizigo yake akatafute shule ambayo
wanasoma bure, Walimu wanofundisha wakiwa hawajalipwa nmishahaara wamekuwa
wakija makao makuu, kwa nini leo hii mwanafunzi anayesoma hapa asilipe ada? Alisema.
Bulembo yuko mkoani Kilimanjaro
katika ziara ya kukagua uhai wa chama na jumuiya zake sambamba na utekelezaji
wa ilani ya uchaguzi wa CCM.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :