TBL YATOA MILIONI 20 KUANDAA MKUTANO MKUU WA SIMBA JUMAMOSI!
Posted in
No comments
Tuesday, July 16, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
Mkutanno Mkuu huo ni fursa safi kwa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, kuwasilisha Ripoti ya shughuli za Klabu hiyo.Simba ambayo ni moja Klabu kigogo na kongwe Nchini, Simba, itafanya Mkutano Mkuu wake
Jumamosi Julai 20 na Mdhamini wao, TBL, Tanzania Breweries Limited,
kupitia Bia yao maarufu Kilimanjaro Premium Lger, imetoa Shilingi
Milioni 20 ili kuendesha Mkutano huo.
TBL, ambayo ina Mikataba ya Miaka mitano
mitano ya kuzidhamini Yanga na Simba kuanzia Miaka miwili iliyopita,
inawajibika kuzipa Klabu hizo Shilingi Milioni 20 kila mmoja ili
kuendesha Mikutano Mikuu ya Vilabu vyao.
Akiongea wakati akikabidhi Cheki ya
Shilingi Milioni 20 kwa Simba, George Kavishe, Meneja wa Bia ya aina ya
Kilimanjaro Premium Lager, alisema: "Kama Wadhamini wakuu, tunatoa Fedha
hizi kama jukumu letu kwa Klabu ili iwajibike, ipate mafanikio nje na
ndani ya Uwanja. Tunaamini Mkutano huu utaimarisha uhusiano kati ya
Simba na Wanachama wake kwa kuwapa nafasi kupitia masuala ya Klabu yao
waipendayo."
Nae Katibu Mkuu wa Simba, Evodius
Mtawala, aliishukuru TBL kwa kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa Mkataba
na akaahidi Fedha hizo zitatumika kama ilivyokusudiwa.
Kwa baadhi ya Wadau wa Simba Mkutano
Mkuu huu unasubiriwa kwa hamu kubwa hasa baada ya Klabu hiyo kugubikwa
na mfarakano na Mwezi Machi Kikundi kimoja cha waliodaiwa kuwa Wanachama
kujaribu kumpindua Rage kwa madai ya kushindwa kuongoza lakini jaribio
hilo halikufua dafu.
Pia, inasemekana ipo Kambi ya Wanachama
itakayoshika bango waelezwe kinagaubaga nini kimetokea kuhusu kuuzwa kwa
Straika wao kutoka Uganda, Emmanuel Okwi, kwa Klabu ya Tunisia Etoile
Sportive Du Sahel Mwezi Januari kwa Dau linalodaiwa kuwa Dola Laki 3 na
Klabu kutolipwa Fedha hizo hadi sasa.
Wengine watapenda wajue nini kiliwasibu
Msimu uliopita na kumalizika Mwezi Mei huku Simba ikinyang’anywa Taji
lao la Ubingwa na Mahasimu wao wakubwa, Yanga, na pia kujikuta
wakibwagwa hadi Nafasi ya 3 nyuma ya Yanga na Azam na hivyo kutopata
fursa ya kucheza Mashindano ya Klabu Barani Afrika Mwakani.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :