MAOFISA WAKAGUZI WASAIDIZI 810 WA JESHI LA POLISI NCHINI WAHITIMU MAFUNZO CCP JANA..

Posted in
No comments
Saturday, November 9, 2013 By danielmjema.blogspot.com


Na Mwandishi Wetu,  Moshi




MAOFISA 810 wamehitimu mafunzo ya uafisa ukaguzi wasaidizi katika chuo cha Mafunzo ya Jeshi la polisi Moshi (MPA)  katika mahafali yaliyofanyika jana katika viwanja vya chuo hicho na kuhudhuriwa na Mkuu wa Jeshi hilo Nchini, IGP Siad Mwema.
 
Kuhitimu kwa Maofisa wakaguzi hao 810 ambao wanaungana na wenzao 600 waliohitmu katika mahafali ya Mwezi wa sita, kunafikisha idadi ya maofisa wakaguzi wa Jeshi hilo kufikia 1410 kwa mwaka huu tu, ambapo kwa jumla hadi sasa jeshi la Polisi nchini linajivunia kuwa zaidi ya Maofisa wakaguzi wapatao 10, 0913.
 
Akizungumza na Wahitimu Hao pamoja na mamia ya Wananchi waliohudhuri sherehe za kufunga mafunzo hayo yaliyodumu kwa takribani miezi sita Mahafali hayo, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP-Said Mwema alisema Jeshi la Polisi nchini linapanga kuifanyia maboresho sera ya Polisi Jamii na Ulinzi shirikishi kwa kupeleka Maaskari wake katika ngazi za Familia na Vijiji, mpango utakaojulikana kama mradi wa usalama katikaFamilia.

IGP-Mwema
IGP Mwema alisema utafiti uliofanywa hivi karibuni na shikrika lisilo la serikali la COSTEC kwa kushirikiana na Wanaharakati mbalimbali nchini pamoja na wanafunzi wa chu kikuu cha Dar es salaam zinaonesha kuwa aslilimia 95 ya wananchi wanakubali sera ya Polisi Jamii na ulinzi shririkishi katika ulinzi na usalama wa Raia na mali yake.

“Utafiti wa Costec, wanaharakati na wanafunzi walioufanya hivi karibuni unaonesha kuwa, zaidi ya asimia 95 ya wananchi wanaikubali sera ya polisi jamii na ulinzi shirikishi katiika ulinzi na usalama wa raia na mali yake,” alisema IGP Mwema
 

Alisema kuwa Jeshi lake limeanza mikakati ya kuhakikisha kuwa ulinzi unaimarika kwa kuboresha sera ya polisi jamii na ulinzi shirikishi kwa kupeleka mradi wa usalama katika ngazi ya familia na kwa kuanzia, Maofisa wakaguzi wasaidizi waliohitimu juzi watapelekwa katika Tarafa zote na vijiji kusadiana na serikali za mitaa kulinda amani.

“Hii ni hatua nzuri, kwa kulitambua hilo jeshi limepanga kuanzisha mradi wa usalama katika ngazi ya familia na kwa kuanzia wahitimu 810 watapelekwa kusimamia mradi huu,” alisema IGP Mwema.

Aidha IGP Mwema aliongeza kuwa katika utekelezaji wa Mradi wa usalama katika ngazi ya familia, Jkwa mwaka huu tu, Jeshi hilo limetenga maaskari zaidi ya 8000 watakaosambazwa nchi nzima.


Kiongozi wa bendi ya CCP, Uncle Vena "Dogo Vena" ambaye ni mwanafunzi katika chuo hicho akitumbuiza mashabiki. Dogo Vena au Uncle Vena aliwahi kukitumikia Bendi ya African Stars Twanga Pepeta kabla ya kuamua kujiunga na chuo cha Polisi CCP.
Awali akitoa ripoti za wahitimu hao kwa Mkuu wa Polisi nchini, IGP Said Mwema, Mkuu wa chuo cha Mafunzo ya Polisi Nchini, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Matanga Mbushi alisema Jumla ya Maofisa 813 walisajiliwa kujiunga na Mafunzo hayo, yaliyoanza Machi 15, Mwaka huu.

ACP Mbushi alisema kati ya hao 813 ni 810 tu ndio waliofanya mitihani na kufaulu huku watatu wakishindwa kumalizia masomo yao akiwemo Askari mwenye namba F713 aliyefariki dunia baada ya kuugua ghafla, wa pili aliacha mwenyewe huku wa tatu akiachishwa kutokana na sababu za kiafya.
 

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .