MWAJUMA KUWAKUTANISHALINEX NA AUNTY EZEKIEL
Msanii Linex Sunday Mjeda aka The V.O.A ameamua
kufungua ukurasa wa pili wa kipaji ambacho hajawahi kukionesha cha
uigizaji, hivi karibuni ataonekana katika filamu mpya ya muigizaji wa
bongo movie Aunty Ezekiel inayoitwa ‘MWAJUMA’.
Kwa mujibu wa tovuti ya bongo5,
linex ameeleza kuwa filamu ya Mwajuma inahusu mwanadada aliyekuwa na
maisha ya chini akiwa mama ntilie na baadae kuja kufanikiwa na kuanza
maisha ya kihuni hususani kubadilisha wanaume kama nguo
Filamu hii inatarajiwa kutoma mwishoni mwa mwezi ujao
No comments:
Post a Comment