UHURU WA KUPENDA NA KUPENDWA UNAVYOATHIRI PENDO HURIA
Posted in
MAKALA
No comments
Friday, March 14, 2014
By
danielmjema.blogspot.com
Uhuru wa kupenda au kupendwa ni moja ya haki binadamu ambayo kama zilivyo haki yoyote ile inatakiwa iheshimiwe kwa sababu kila mmoja ana haki ya kuoensha hisia zake katika kile ambacho moyo wake unaouhusudu.
Uhuru huu wakati mwengine
hutafsiriwa kutokana na Dini, kabila au utamaduni wa jamii kwa mujibu wa sheria
za nchi au eneo husika.
Kuna kitu upendo na kuna kitu
uhuru, uhuru kidunia ni uwezo wa kufanya utakacho, utakavyo, utakapo na kwa umtakaye,
lakini ifahamike kuwa falsafa inatukumbusha kuwa endapo mtu atakuwa na uhuru wa
kufanya kitu vilevile anakuwa na uhuru wa kutokifanya.
Miktadha ni mingi maana katika
kupenda kuna kupenda kitu, gari na uturi au kumpenda mtu mfano mapenzi kati ya
wazazi na wana wao au ndugu lakini pia kuna mapenzi ya yaliyozoeleka kama muhibu,
nyonda, mpenz, laazizi, kichuna, uyuni ambao tunakesha kila siku kuwatungia
mashairi na kuwasifu katika nyimbo.
Lakini katika kujivunia uwepo wa
mazingira yoyote yale ya haki ya kupenda au kupendwa, Uhuru na pendo
zikichanganyika migogoro, balaa uvunjifu wa amani au hata mauaji huwezi kutokea
maana uhuru wa kupenda au kupendwa ni tofauti na pendo huria.
Pendo huria mara nyingi
hukwaruzana na uhuru wa kupenda, ni vigumu kufanya kitu kwa sababu kuna uhuru
wa kupenda au kupendwa, huwezi kumalimisha mtu kumpenda mtu au kupendwa na mtu
tu eti kwa sababu kuna uhuru wa kufanya hivyo, kwa kufanya hivyo kutakuwa na
kitu kinaitwa Mapenzi elekezi.
Moja ya matukio kama haya yaliwahi kuripotiwa hapa nchini na hata nchi jirani ya Kenya ambapo katika kijiji cha ngamwa mukurweini, kaunti ya Nyeri kati ya familia ya Geofrey Kibuyi na mke wake.
Katika tukio hilo Jane Wamboi ambaye ni mke wa Kibuyi alifikishwa Hospitalini baada ya kudaiawa kunywa sumu.
Jamii nyingi imejikuta ikitumia
uhuru huu kuvunja dhana ya pendo huria, tamaduni nyingi ya kiafrika kwa mfano
ni wahanga wa pendo elekezi au pendo shuruti, utamsikia baba akimwambia mwanaye
sisi kama wazazi wako tumeridhikana mtu Fulani hivyo wewe unachopaswa kufanya
ni kufuata na kutii na sio kuhoji.
Katika mfano kama huu mara nyingi
wanawake wamekuwa ni wahanga wakubwa sana, hali hii ni tatizo kubwa ambalo
limekuwa likizalisha ndoa zisizokuwa na amani ambapo wahanga wakubwa wamekuwa
na wanawake na watoto.
Mwisho.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :