 |
| Mkuu wa Polisi wilaya ya Monduli, OCD Mourice Okinda akisalimiana na baadhi ya wanariadha muda mfupi kabla ya mbio za Sokoine Mini Marathon kilomita 10 kuanza. |
 |
| Waziri mwenye Dhamana na michezo, Dkt. Fenela Mukangara akianzisha mbio za Kilomita 10 |
 |
| Wanariadha wakichuana katika mbio za Sokoine Marathon 2014 kilomita 10 zilizofanyika jana kama sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 30 ya kifo cha Sokoine |
 |
| Njia ilikuwa imejaa tope kufuatia mvua kubwa zilizonyesha |
 |
| Fabian Joseph akimaliza mbio za Kilomita 10. Joseph alishinda mbio hizo |
 |
| Mshindi wa pili Alphonce Felix wa Holili akimaliza mbio |
 |
| Dickson Marwa wa Holili akimaliza mbio za mwaka huu. mwaka jana al;ikuwa mshindi mwaka huu kaja wa tatu |
 |
| Mshindi wa mbio kilomita 10 wanawake, Javkline Sakilu akimaliza mbio hizo. Jackline Jackline Sakilu, kutoka klabu ya Winning Spirit ya
Arusha, aliibuka mshindi akitumia muda wa dakika 40:01:26,alitumia muda wa dakika |
 |
| Nathalia Elisante wa Arusha akimaliza mbio katika nafasi ya pili, akitumia muada wa ambaye alitumia muda wa dakika 40:51:2. |
Na Mwandishi wetu, Monduli
Mwanariadha Fabian Joseph kutoka Arusha alishinda mbio za kilomita 10
kwa upande wa Wanaume akitumia muda wa dakika 34:28.04 akimpita
mwanariadha chipukizi Alphonce Felix zikiwa zimesalia kilomita moja
mbio hizo zimalizike.
Nafasi ya Pili ilienda kwa, Alphonce Felix kutoka katika klabu ya
Holili, ambaye alitumia muda wa dakika 34:45.39 huku bingwa mtetezi
Dickson Marwa kutoka holili akiridhika na nafasi ya tatu akitumia muda
wa dakika 34:57.47.
Kwa upande wa mbio za wanawake, Bingwa wa mbio za Kilimanjaro marathon
kilomita 21, Jackline Sakilu, kutoka klabu ya Winning Spirit ya
Arusha, aliibuka mshindi akitumia muda wa dakika 40:01:26, huku
anafasi ya pili ikienda kwa Nathalia Elisante wa Arusha ambaye
alitumia muda wa dakika 40:51:27 na nafsi ya tatu ikashikiliwa na
Failuna Abdi, wa winning spirit, aliyekimbia kwa dakika 41:13:54.
No comments:
Post a Comment