ALIYETAKA KUMTAPELI DKT. SLAA KESI YAKE YAPIGWA KALENDA

Posted in
No comments
Friday, May 2, 2014 By danielmjema.blogspot.com


Na Mwandishi wetu, Hai

Usikilizwaji wa kesi ya jaribio la kumtapeli katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, umekwama baada ya hakimu anayeisikiliza kupata udhuru.

Jaji mkuu mstaafu,Barnabas Samatta, Mbunge wa Arusha mjini,Godbless Lema na wakili wa Chadema, Profesa Abdalah Safari ni miongoni mwa mashahidi 12 watakaotoa ushahidi katika kesi hiyo.

Kesi hiyo inayovuta hisia za wakazi wa miji ya Arusha na Moshi, ilikuwa imepangwa kuanza kusikilizwa Ijumaa iliyopita mbele ya hakimu mkazi wa wilaya ya Hai, Denis Mpelembwa.Hata hivyo kesi hiyo iliahirishwa baada ya Hakimu kuwa nje ya ofisi kikazi.

Inadaiwa kati kati ya Aprili na Mei, 2012, mshitakiwa Abedi adamu Abeid (23), alijitambulisha kwa Dk. Slaa, Lema na Profesa Safari kuwa yeye ni mkuu wa Takukuru wilaya ya Ulanga, Abel Kibaso.

Katika kipindi hicho pia, mtuhumiwa aliwapigia simu viongozi hao akijitambulisha ni Jaji mstaafu Samatta akitaka wampe pesa ili washinde katika kesi namba 47/2012 iliyokuwa mahakama ya Rufaa.

Rufaa hiyo  ilifunguliwa na Lema dhidi ya Mussa Hamisi na wenzake akipinga hukumu ya mahakama kuu Arusha ya kumvua  Ubunge wa Arusha mjini.

Hata hivyo Lema alishinda Rufaa hiyo na kurudishiwa Ubunge wake.waendesha mashitaka kutoka taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (takukuru) wanadai mtuhumiwa alijifanya ni Jaji mkuu mstaafu Samatta wakati akijua siyo Jaji Samatta kwa lengo tu la kujipatia fedha kinyume cha sheria.

Mshitakiwa amekanusha mashitaka hayo na sasa kesi hiyo imepangwa kusikilizwa Mei 21 baada ya kukwama kusikilizwa Ijumaa iliyopita.

Mwisho
 

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .