LEO NI KUMBUKUMBU YA MIAKA 18 YA MV BUKOBA

Posted in
No comments
Wednesday, May 21, 2014 By danielmjema.blogspot.com

Leo imetimia miaka 18 tangu ndugu zetu walipopata ajali na Meli ya MV. Bukoba 21 May 1996, na wengi kupoteza maisha! Ni tukio kubwa lililoua watu wengi nchini na kuacha huzuni kubwa kwa Watanzania.
Comment R.I.P kwao ili waendelee kupumzika kwa amani!
Mei 21,1996 katika ziwa Victoria,Mwanza Tanzania meli ya Mv Bukoba ilipata ajali na zaidi ya watu 800 kupoteza maisha yao.Meli ilizama kilomita 30 kukaribia kutua nanga kwenye bandari ya mwanza ikitokea Bukoba. Meli ikuwa na uwezo wa kubeba idadi ya watu 430. 



Kwenye first and second class orodha ya abiria ilikuwa 443 na kwenye third class hakukuwepo rekodi yoyote .Takribani 1000 walifariki kwenye ajali hiyo.

Afrika ya kusini ilibidi kutoa msaada wa wanamaji wake waje kutusaidia kufanya uzamiaji wa kina kirefu kwani tulikuwa hatuna hivyo vifaa na utalaamu(sijui inagharimu kiasi gani kuvipata vifaa na utalaamu)

Meli ilikuwa na ubovu lakini iliruhusiwa kuendelea na kazi kama kawaida.(nani anajali au kuwajibishwa?)


Vifaa vya uokoaji mfano majaketi(life jacket) n.k na vitu kama hivyo vilikuwepo vya kutosha?( au hakuna uzembe wa viongozi..ni kazi ya Mungu kama walivyozoea kusema)


SWALI LA MSINGI!!!!!
hivi Serikali imeshindwa kutenga japo dakika 3 nchi nzima kusimama kuwakumbuka ndugu zetu waliotutoka kutokana na uzembe wa watendaji wa serikali?

Kama wanaweza kukusanya mamilioni kusherekea sherehe za kisiasa inagharimu nini kutoa tamko kuhusu hiyo siku.

Poleni sana wafiwa..tupo pamoja ..mwenyezi Mungu awapumzishe mahala pema peponi woote waliotangulia mbele ya haki.Amina

REST IN PEACE

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .