MTEMVU ATOA MKONO WA IDD WA VYOMBO NA SH. 10,000 KWA VIONGOZI 912 WA MATAWI YA CCM TEMEKE

Posted in
No comments
Tuesday, July 29, 2014 By danielmjema.blogspot.com

Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (kulia), akimkabidhi boksi la vyombo na zawadi ya sh. 10,000 mmoja wa viongozi 912 wa matawi wa ya CCM na jumuiya zake wa jimbo hilo, katika hafla ya kutoa mkono wa Idd el Fitr Dar es Salaam jana. Kila mmoja alipata zawadi kama hiyo. Katika boksi hilo kuna vikombe, birika, vijigo, sahani na chupa ya chai. Katikati ni mke wa mbunge huyo, Mariam Mtemvu. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Mtemvu akimkabidhi Mwenyekiti wa UWT CCM tawi la Mji Mpya Kata ya Buza, Temeke.

Baadhi ya viongozi wakiondoka na vyombo vyao huku wakiwa na sh. 10,000 kibindoni.
Shehena ya vyombo vilivyokuwa vinagawiwa
Sehemu ya umati wa viongozi wa CCM wa matawi waliofika kupata zawadi hizo. Wengi walimpongeza Mtemvu kwa moyo wake wa kujitolea.
Ni furaha tele kwa mama huyo

        Mary wa Yombo Kilakala akifurahia zawadi yake na kitita cha sh. 10,000
Mwenyekiti wa CCM Tawi la Mlimani, Kata ya Kilakala, Temeke, Dar es Salaam, Omar Kichapwi huyoooo na vyombo vyake . ndani ya vyombo hivyo kuna vikombe, birika vijiko na chupa ya chai
Mke wa Mbunge wa Jimbo la Temeke, Mariam Mtemvu akimkabidhi zawadi ya vyombo na sh. 10,000 mmoja wa viongozi wa CCM wa Jimbo hilo.
Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke,  akimkabidhi vyombo na sh. sh. 10,000 mmoja wa viongozi wa matawi wa CCM wa Jimbo hilo. Zawadi hizo zilitolewa na Mbunge wa Jimbo hilo, Abbas Mtemvu (kulia).
Wakifurahia kupata zawadi hizo

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .