WAZIRI WA FEDHA, MHE. SAADA MKUYA ATEMBELEA MANISPAA ZA ILALA, KINONDONI NA TEMEKE

Posted in
No comments
Friday, July 18, 2014 By danielmjema.blogspot.com

 Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Bw. Stima Kabikile (katikati) akimkaribisha rasmi Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kulia) wakati alipofanya ziara yake ya siku moja katika Manispaa za Ilala, Kinondoni na Temeke kwaajili ya kupata taarifa kuhusu kodi za majengo na utendaji kazi wa wataalam wanaoshughulikia masuala hayo na mbinu za kuboresha namna ya ukusanyaji kodi hizo ili kuwarahisishia walipaji kodi.
 Waziri wa Fedha, Bi Saada Mkuya akiweka saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi za Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kwaajili ya ziara yake ya siku moja ndani ya jiji la Dar es salaam kwaajili ya kupata taarifa kuhusu kodi za majengo na utendaji kazi wa wataalam wanaoshughulikia masuala hayo na mbinu za kuboresha namna ya ukusanyaji kodi hizo ili kuwarahisishia walipaji kodi.
 Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya (kulia) Ilala akimsomea taarifa ya makusanyo ya kodi za majengo na mikakati  yake ya kufikia malengo waliojipangia ili kuongeza mapato Mhe. Waziri wa Fedha Bi. Saada Mkuya wakati wa ziara ya siku moja katika Manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni.
 Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya akipitia moja ya taarifa alizopewa na uongozi wa Halmashauri wilaya ya Kiondoni wakati alipofanya ziara yake ya siku moja ofisi hapo. 
 Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mwandisi Mussa Natty (kulia) akimpokea Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kushoto) wakati alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi ya Manispaa hiyo jana kwaajili ya kupata taarifa mbalimbali kuhusu makusanyo ya kodi za majengo pamoja kupeana mikakati mizuri ya kuboresha mifumo ya ukusanyaji kodi hizo ili kuwarahisishia kazi walipaji kodi ambao ni wananchi.
 Mtathmini wa Manispaa ya Temeke Bw. Victor Ndonne (kushoto) akimuonyesha nyaraka za makusanyo ya kodi za majengo Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (aliyekaa katikati) wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja katika Manispaa hiyo.
 Baadhi ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo wakisikiliza maelezo mazuri toka kwa Waziri wa Fedha kuhusu namna ya kuboresha makusanyo ya kodi za majengo kwa kujikita na matumizi ya TEHAMA katika ukusanayaji wa kodi hizo kama njia rahisi ya kuwarahisishia walipaji kodi.
 Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kulia) akiongozana na viongozi wa Manispaa ya Kinondoni wakati alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi ya Manispaa hiyo jana kwaajili ya kupata taarifa mbalimbali kuhusu makusanyo ya kodi za majengo pamoja kupeana mikakati mizuri ya kuboresha mifumo ya ukusanyaji kodi hizo ili kuwarahisishia kazi walipaji kodi ambao ni wananchi. katikati ni Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Bw. Yusuph Mwenda na kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mwandisi Mussa Natty.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Bw. Photidas Kagimbo (kulia) akisalimiana na Waziri waFedha, Mhe. Saada Mkuya (kushoto) mara alipowasili katika ofisi za Manispaa hiyo kwa ziara ya kikazi katika jana kwaajili ya kupata taarifa mbalimbali kuhusu makusanyo zikiwemo njia wanazotumia kukusanya kodi za majengo pamoja kupeana mikakati mizuri ya kuboresha mifumo ya ukusanyaji kodi hizo ili kuwarahisishia kazi walipaji kodi ambao ni wananchi.
 Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kulia) akihutubia mkutano huku akisisitiza juu ya kujikita zaidi katika kutumia TEHAMA katika kukusanya kodi za majengo kama njia rahisi inayomrahisishia mlipaji kodi kuweza kulipa kodi zake katika vituo vya huduma.
 Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kushoto) akiweka saini katika kitabu cha wageni mara alipowasili ofisi za Manispaa ya Kinondoni kwaajili ya ziara ya kikazi jana kwaajili ya kupata taarifa mbalimbali kuhusu makusanyo ya kodi za majengo pamoja kupeana mikakati mizuri ya kuboresha mifumo ya ukusanyaji kodi hizo ili kuwarahisishia kazi walipaji kodi ambao ni wananchi. Kulia ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Bw. Yusuph Mwenda.
 Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Bw. Yusuph Mwenda (kulia) akitoa maelezo yake kwa Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kushoto) wakati wa mkutano na viongzoi wa Manispaa ya Kinondoni jana jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya akitoa hotuba fupi yenye kuwaelekeza viongozi wa Manispaa ya Kinondoni  huku akiwasisitizia kutumia mifumo ya TEHAMA katika kuleta ufanisi ukusanyaji kodi kama njia rahisi inayowasaidia walipaji kodi kutopata usumbufu wakati wa ulipaji.
Wajumbe kutoka Manispaa ya Temeke wakisikiliza kwa makini maelezo yakiyotolewa na Mkurugenzi wao (hayupo pichani) kuhusu taarifa aliyokuwa akiwasilisha jana katika Manispaa hiyo.
Picha zote na Benedict Liwenga

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .