KAMPENI ZA DK MAGUFULI KWAO CHATO NI ZAIDI YA TSUNAMI

No comments
Wednesday, September 23, 2015 By danielmjema.blogspot.com


Mgombea urais wa Tbanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli akiwapungia mkono wananchi wakati wa mkutano wa kampeni za urais, ubunge na udiwani kwenye Uwanja wa Michezo mjini Chato, mkoani Geita, jimbo alilokuwa Mbunge. Pia alitumia fursa hiyo kuwaaga wapiga kura wake.Mkutano huo wa kampeni ulijaza watu kupita kiasi  jambo ambalo wenyeji wa wilaya hiyo pamoja na mgombea amesema haijawahi kutokea.PICHA ZOTE NA RICHARD BMWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Mbuzi huyu aliyechorwa maandishi hayo aliletwa kwenye mkutano huo na mmoja wa wafuasi wa CCM kwa lengo la kuwakebehi Ukawa.
Dk. Magufuli akijinadi kwa wananchi wa Wilaya ya Chato ili wampigie kura nyingi yeye pamoja na mbunge na diwani wa CCM.
Dk Magufuli akiwahidi wananchi kuwa akipewa ridhaa ya kuongoza nchi atahakikisha  elimu ya bure inatolewa kuanzia shule za msingi hadi kidato cha nne
Mke wa  Mgombea urais wa Tganzania kupitia CCM, Janeth Magufuli akipongezwa na mumewe, Dk Magufuli baada ya kutoka kumuombea kura 

Wasanii wa muziki wa kizazi kipya wakitumbuiza wakati wa mkutano huo

Baadhi ya wananchi wakiwa na mabango yenye ujumbe tofauti

Baadhi ya wapigapicha za habari wakiwa juu ya magari kwa lengo la kupata picha nzuri wakati msafara wa Dk Magufuli ulipokuwa ukitokea nyumbani kwao kwenda kwenye mkutano wa kampeni kwenye Uwanja wa Michezo mjini Chato leo

Dk Magufuli akiingia kwenye mkutano wa kampeni mjini Chato

Kikundi cha ngoma za asili cha Mchele Mchele kikitumbuiza katika mkutano huo
Wanamuziki wa Yamoto Band wakitumbuiza  wakati wa mkutano huo

Wafuasi wa CCM wakionesha dole gumba ikiwa ni ishara ya kumkubali Dk Magufuli kuwa rais
Msanii Khadija Kopa wa Kikundi cha Sanaa cha CCM cha TOT, AKITUMBUIZA KWA WIMBO WA TAARABU WAKATI WA KAMPENI HIZO
Wasanii wengine wakiendelea kuunga mkono Malkia wa Mipasho Khadija Kopa

Mjumbe wa Kamati ya Kampeni za CCM, Abdallah Bulembo akielezea wasifu wa Dk. Magufuli uliomfanya ateuliwe na CCM kuwa mgombea urais wa Jamhuri ya Tanzania.
Dk Magufuli akizungumza na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Josph Musukuma wakati wa kampeni hizo
Mwakilishi wa watu wenye ulemavu wana CCM na wasio wanaCCM, Amon Mpanju akihutubia kwa kuelezea ubaya wa Ukawa na kusifia CCM ambayo alidai inawajali walemavu nchini.
Dk Magufuli akiwa na baadhi ya viongozi wakiangalia vikundi vya sanaa vilivyokuwa vikitumbuiza katika mkutano huo
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Jpseph Musukuma akimwagia sifa lukuki Dk. Magufuli kuwa anafaa kuwa urais na kumponda mgombea urais  kupitia Ukawa ambaye alisema hafai kwani afya yake
Mke wa Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Janeth Magufuli akipita jukwaani baada ya kutoka kuhutubia na kuwaomba wananchi kumpigia kura mumewe ili ashinde urais wakati wa mkutano wa kampeni kwenye Uwanja wa Michezo mjini Chato.

Dk Magufuli akijipigia kampeni nyumbani kwao Chato
Dk Magufuli akiwaaga wananchi baada ya mkutano wa kampeni kumalizika  mjinbi Chato


Msafara wa Dk Magufuli ukipita kwenye taa za kuongozea magari ambazo alifanikisha kuziweka alipokuwa mbunge wa Jimbo la Chato




Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .