RIPOTI YA DUNIA YAITAJA SERIKALI YA RWANDA KUONGOZA KWA UTENDAJI AFRIKA MASHARIKI

No comments
Thursday, March 31, 2016 By danielmjema.blogspot.com


Rwanda imeorodheshwa kuwa nchi ya 7 duniani kwa kutoa huduma za haraka na rahisi za serikali. Ripoti iliyotolewa na baraza la Uchumi duniani imeiorodhesha Rwanda mbele ya Malaysia, Uswisi na Luxembourg ambazo zilichukua nafasi za 8, 9 na 10. 

Utafiti wa baraza hilo pia umeonesha kuwa serikali ya Qatar ndio iliyo na utendaji bora zaidi ikifuatiwa na Singapore na Finland.

Akiongea na waandishi wa habari mkurugenzi wa Bodi ya utawala ya Rwanda Bwana Anastase Shyaka amesema nchi yake inafanya juhudi kubwa kukuza uwazi na uwajibikaji kwenye mfumo wake, na raia wengi wana habari kuhusu jinsi serikali inavyofanya kazi na kutoa maamuzi. 

Kwingineko barani Afrika Mauritius iko kwenye nafasi ya 26 na kama Afrika Kusini iko katika nafasi ya 32 Kenya na Tanzania Je?

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .