Uswisi kuzindua Reli ndefu zaidi Duniani inayopita 'underground' imejengwa kwa miaka 17

Posted in
No comments
Wednesday, May 25, 2016 By danielmjema.blogspot.com

Baada ya kutangaza mpango wa kuwalipa vijana wote (wa kiume na kike) ambao wamefikiwa umri wa kufanya kazi na hawana kazi, posho ya kujikimu, ya kiasi cha dola 2500 kila mwezi, Uswisi imeingia kwenye vichwa vya habari tena.
Kwa sasa taarifa kubwa inayotikisa kutoka Uswizi ni kwamba, Reli ndefu zaidi ambayo inapita chini ya ardhi imepangwa kufunguliwa wiki za hivi karibuni baada ya miaka 17 ya ujenzi, reli hiyo kwa mara ya kwanza ilianza na mchoro mwaka 1947 lakini ujenzi wake ulianza miaka 17 iliyopita.
Majaribio ya treni kwenye reli hiyo yanatarajiwa kuanza wiki ijayo June na abiria wa kwanza kabisa kwenye treni hiyo wanatarajiwa kuanza December, Miamba tani milioni 28.2 imetumika kujengea reli hiyo.
Imeelezwa kwamba kuanzishwa kwa reli hiyo kutasaidia suala zima la usafiri ambapo Muda wa kusafiri kati ya Zurich na Millan utapungua kutoka masaa mawili na dakika 40 na itakuwa saa moja ambayo ni haraka zaidi  ukilinganisha na ilivyo hivi sasa.

  

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .