WILFRED MOSHI AMERUDI NCHINI LEO BAADA YA KUWEKA REKODI YA KUFIKA KATIKA KILELE CHA EVAREST

Posted in
No comments
Wednesday, May 30, 2012 By danielmjema.blogspot.com



KIJANA Wilfred moshi(33), mkazi wa moshi mjini, wilaya ya moshi, mkoani Kilimanjaro ambaye ni mtanzania wa kwanza kufika katika kilele cha mlima Evarest amerejea nchini na kupokelewa na umati mkubwa ya watanzania waliofurika katika uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro KIA, kumpokea shujaa aliyeandika historia kwa kufika kilele cha mlima huo mrefu zaidi duniani.
Wilfred ambaye ni mfanyakazi wa kampuni ya kitalii cha Nature Discovery amerejea nchini ikiwa ni siku chache tu  tangu alipofanikiwa kufika katika kilele cha mlima Evarest tarehe 19 ya mwezi huu. Wilfred alipokelewa uwanjani hapo na ndugu jamaa na marafiki wakiwemo baba yake mzazi Ceryl Moshi, mama yake mzazi Martina moshi, mke wake Agness Wilfred pamoja na watoto wake wawili Martina Wilfred na Martin Wilfred.
Akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kutua katika ardhi ya Tanzania, Wilfred aliyeondoka hapa nchini Machi 28 mwaka huu akielekea Newzealand alisema baada ya kufika Newzealand aliungana na marafiki zake na kufunga safari kuelekea Nepal ambako ndiko iliko mlima Evarest. alisema  katika safari yao walikumbana na vikwazo vingi sana akitaja tatizo la hewa kuwasumbua sana hadi kulazimika kutumia hewa ya oksijeni.
“namshukuru sana Mwenyezi kwa kufanikisha  ndoto yangu ya kuwa mtanzania wa kwanza kuingia katika kumbukumbu za vitabu kufika katika kilele cha mlima evarest, siri ya mafanikio siku zote ni kujituma na kuwa na imani katika kile unachokifanya .naiomba serikali, adau wote wa katika sekta ya utalii, wizara ya utamaduni, waangalie ni kwa namna gani tunaweza kufanya katika kuhakikisha tunaitangaza vyema nchi yetu pamoja na rasilmali zake zote pamoja na kuenzi mlima wetu, mlima kilimanjaro,” alisema Wilfred.
Wakiongea na MTANZANIA kwa nyakati tofauti, baadhi ya wananchi waliofika uwanjani hapo kumpokea shujaa wao, waliitaka serikali na wahusika  katika idara zake zote kuhakikisha kwamba kile kilichofanywa na mzalendo Wilfred hakipotei hivihilivi. walisema kwa kulipeperusha bendera ya Tanzania ni vyema wizara ya utalii pamoja na ile ya utamaduni kumtangaza kijana Wilfred moshi kuwa balozi wa kulitangaza mlima Kilimanjaro katika anga la kimataifa.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .