WATUHUMIWA WA NOTI BANDIA MBARONI KILIMANJARO

Posted in
No comments
Monday, July 23, 2012 By danielmjema.blogspot.com

JESHI la polisi Mkoani Kilimanjaro, limekamata Noti Bandia za sh. 10,000 zenye Thamani ya sh. 600,000 fedha za Kitanzania na kushikilia watuhumiwa wawili katika tukio hilo lilitokea katika maeneo ya kituo cha petroli cha Karanga, Manispaa ya Moshi, Mkoani Kilimanjaro.

Kwa mujibu wa taarifa za Polisi kwa vyombo vya habari, Watuhumiwa hao Husna Karimu(36) ambaye ni mkazi wa Majengo-Dar es salaam na Hamza Mohamedi (60), Mkulima, Mkazi wa Mijongweni, Mkoani Kilimanjaro, walifika dukani kwa Sharifa Saidi ambaye ni mfanyabiashara wakihitaji kupewa huduma ya kutuma pesa kwa njia ya M-pesa.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa upelelezi mkoani Kilimanjaro, Ramadhani Ng’anzi, alisema kwamba watuhumiwa  hao walikamatwa mnamo tarehe 21 julai mwaka huu, wakiwa na noti 22 za Tshs. 10,000 zenye namba BF1547948 na Noti 17 za Tshs. 10,000 zenye namba BC2937831.

Alisema kwamba, Mtuhumiwa wa kwanza ambaye ni Mkazi wa Majengo Jijini Dar es salaam, mpaka sasa haijafajhamikka mara moja shughuli maalum iliyomleta mkoani hapo lakini uchunguzi zaidi unaendelea na mara baada ya kupata vielelezo kamili, hatua za kisheria zitafuta mkondo wake ikiwa ni pamoja na kuwafikisha Watuhumiwa hao Mahakamani.

Aidha, Jeshi la Polisi Mkoani Kilimanjaro lilitoa tahadhari kwa Wananchi hasa Mawakala wa Makampuni ya Simu za mkononi kwa njia ya Mtandao wa Makampuni hayo kwamba kuna Wimbi la utoaji wa Noti za Bandia, hivyo wawe makini na kushirikiana na Vyombo vya Usalama katika kuhakikisha wimbi la Matukio kama hayo yanayoanza kujitokeza yanakomeshwa.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .