KLABU YA WANAHABARI MKOANI KILIMANJARO (MECKI), WALAANI UKATILI ALIOFANYIWA MWENYEKITI WA JUKWAA LA WAHARIRI, ABSALOM KIBANDA.
Posted in
No comments
Saturday, March 16, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
KLABU ya
waandishi wa habari mkoa wa Kilimanjaro(MECKI) imeungana na
taasisi,wanaharakati na watu wengine, kulaani tukio la kuvamiwa, kupigwa na
kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda. | |||
Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa New Habari 2006, alijeruhiwa usiku wa kuamkia Machi 9, mwaka huu na watu ambao hadi sasa hakuna taarifa ya kufahamika kwao.
Klabu inalaani kwa nguvu zote mashambulizi yote, ambayo yamefanywa kwa wanahabari katika kipindi cha takribani miaka miwili mfululizo ambayo, baadhi yake yamesababisha vifo kwa wanahabari hao na wengine kupata ulemavu maishani mwao.
Akitoa
tamko hilo la wanahabari wote mkoani Kilimanjaro, Mwenyekiti wa MECKI,
Rodrick Makundi alikumbusha kwamba ni Jukumu la wanahabari na vyombo vya
habari wanavyoviwakilisha, kuelemisha jamii na kuwasaidia
wananchi katika kutiririsha mawazo katika nyanja mbalimbali, kulenga kuleta uhuru wa kweli na kujenga demokrasia hata pale inapotokea kukawa na kutofautiana kwa hoja ili mradi sheria
za nchi hazivunjwi.
"
Ikumbukwe
kwamba ni Jukumu letu sisi kama wanahabari na vyombo vya habari tunavyoviwakilisha, kuelemisha jamii na kuwasaidia
wananchi katika kutiririsha mawazo katika Nyanja mbalimbali, sote tukilenga kuleta uhuru wa kweli na kujenga demokrasia hata pale tunapotofautiana kwa hoja ili mradi sheria
za nchi hazivunjwi,"
Aidha aliwataka Waandishi wa Habari, kutumia tukio hilo kama chachu katika kupigania maslahi ya wananchi na rasilimali za
nchi ili ziweze kuwanufaisha wote kwa
ujumla na si wachache ambao kwa bahati mbaya wamesahau maadili ya utumishi wa
umma.
Klabu inatoa
rai kwa serikali kupitia vyombo vyake vya dola, kufanya uchunguzi wa kina wa
tukio hilo na yale yaliyopita na wahusika watakaokamatwa wachukuliwe
hatua kali za kisheria,kwani mashambulizi
dhidi ya wanahabari ni tishio kwa demokrasia.
Naye Katibu wa MECKI, James Nakajumo, aliitaka jamii isaidie kufichua hujuma dhidi ya wanahabari kwani tukio la kutekwa na kuteswa kwa Kibanda ni miongoni mwa matukio zaidi ya matano yaliyotokea katika kipindi kifupi kilichopita.
Alisema Klabu inatoa pole kwa Kibanda, familia yake na tasnia ya habari kwa ujumla, lakini kubwa zaidi ni kuomba watanzania kumuombea kwa MUNGU ili aweze kupona haraka na arejee salama katika shughuli za ujenzi wa taifa.
Naye Katibu wa MECKI, James Nakajumo, aliitaka jamii isaidie kufichua hujuma dhidi ya wanahabari kwani tukio la kutekwa na kuteswa kwa Kibanda ni miongoni mwa matukio zaidi ya matano yaliyotokea katika kipindi kifupi kilichopita.
Alisema Klabu inatoa pole kwa Kibanda, familia yake na tasnia ya habari kwa ujumla, lakini kubwa zaidi ni kuomba watanzania kumuombea kwa MUNGU ili aweze kupona haraka na arejee salama katika shughuli za ujenzi wa taifa.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :