Wasanii wa Injili kushiriki tamasha la Tumaini Jipya Machi 31 mkoani Morogoro, Martha Mwaipaja, Stara Thomas, Masanja Mkandamizaji Ndani!
Posted in
No comments
Thursday, March 21, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
KAMPUNI ya QS Entertainment, imeandaa tamasha kubwa la ‘Tumaini
Jipya’ linalotarajiwa kufanyika Machi 31 kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro likihusisha waimbaji
mbalimbali hapa nchini.
Mkurugenzi-Mhonda |
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya QS Entertainment, Joseph
Mhonda alisema kuwa tamasha hilo lina lengo la kuwasaidia watu wenye
mahitaji maalumu kwenye jamii
ikiwemo
watoto yatima na kutarajiwa pia kufanyika katika mikoa mbalimbali baada
ya
kuzinduliwa mkoani Morogoro likiwa na lengo kubwa la kueneza neno la
bwana na mambo mengine ya kijamii katika kila mkoa watakapokuwapo.
Martha Mwaipaja akizungumza
jambo na mwimbaji mwingine wa muziki wa Injili, Stara Thomas, aliyewahi kuwika
pia kwenye muziki wa Kidunia, maarufu kama Bongo Fleva.
=
Martha Mwaipaja,
akizungumza jambo.
Mkurugenzi wa Kampuni
hiyo, Joseph Mhonda, ambao ndio waandaaji wa tamasha akiwa mbele ya kamera ya Handeni Kwetu Blog.
Mkurugenzi wa QS Entertainment, Joseph Mhonda, akizungumza katika utambulisho wa Tamasha la Tumaini Jipya.
Mhonda,
amesema kuwa amejipanga imara kuhakikisha kuwa tamasha lao la ‘Tumaini Jipya’
linalotarajiwa kufanyika Machi 31 kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, linagusa hisia za wengi kwa
kushirikisha wakali mbalimbali wa muziki wa Injili nchini.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mhonda alisema kuwa
alisema kuwa tamasha hilo lina lengo la kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu kwenye jamii ikiwemo watoto yatima na
kutarajiwa pia kufanyika katika mikoa mbalimbali baada ya kuzinduliwa mkoani
Morogoro.
Martha Mwaipaja
“Tamasha hili limeanzia Morogoeo lakini litaendelea kwenye m
ikoa mingine ya Tanzania likiwa na lengo
la kutoa tumaini kwa jamii, na mapato
yatakayopatikana yatasaidia watu walio
katika mazingira magumu” alisema Mhonda
Alisema katika tamasha hilo ambalo ni la aina yake kufanyika
Tanzania, litapambwa na waimbaji wakubwa wa muziki wa Injili Afrika Mashariki
ambao ni Bahati Bukuku, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’, Joseph Nyuki,
Stara Thomas, Matha Mwaipaja, Sifa John, Chamwenyewe na Revina Steven.
Stara Thomas akiteta jambo na Martha Mwaipaja
Mbali na waimbaji hao
pia kutakuwa na kwaya mbalimali Rafiki Gospel Singers, Haleluya Kwaya,
Victoria Kwaya na MTC .
Mhonda alisema sambamba na kutoa burudani ya mziki kupitia
waimbaji hao pia watakuwa na muda maalum wa kutoa elimu ya Ujasiriamali kwa
watu wote, pamoja na mbinu za kufaulu mtihani kwa wanafunzi.
Kwa mujibu wa waandaaji hao, Tamasha la Tumaini Jipya, ni fursa
pekee kwa wakazi wa Morogoro kuweza kujumuika na watu wengine duniani katika
kusherehekea siku Kuu ya Pasaka.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :