LIVERPOOL YAPIGA CHINI OFA YA PAUNI 40 ZA ARSENAL KWA SUAREZ
Posted in
No comments
Wednesday, July 24, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
LIVERPOOL
imeikataa Ofa nyingine ya Arsenal ya Pauni Milioni 40,000,001 kwa ajili
ya kumnunua Straika kutoka Uruguay, Luis Suarez.
Ofa hii, yenye idadi ya Fedha ya ajabu
kidogo, ni ya makusudi ili ‘kuamsha’ Kipengele cha Mkataba wa Suarez
ambacho kinaitaka Liverpool kutafakari Ofa yeyote ya kumnunua Suarez
itakayotolewa ikiwa tu imevuka Pauni Milioni 40 na pia ni wajibu
Mchezaji huyo kujulishwa kuhusu Ofa hiyo.
Lakini, Kisheria, Liverpool hawawajibiki kumuuza na hivyo ndivyo walivyofanya kwa kuikataa Ofa hii ya sasa ya Arsenal.
Arsenal, ambao Rekodi yao ya juu kabisa
kumnunua Mchezaji ni Pauni Milioni 15 walizoilipa Zenit St Petersburg
kwa ajili ya Andrey Arshavin Januari 2009, walitoa Ofa ya kwanza kwa
Liverpool ya Pauni Milioni 30 na kukataliwa na Liverpool.
Wiki iliyopita Meneja wa Liverpool,
Brendan Rodgers, alisema thamani halisi ya Luis Suarez ni sawa na
Edinson Cavani ambae hivi karibuni alijiunga na Paris St-Germain kwa Dau
la Pauni Milioni 55.
Mbali ya Arsenal kumwandama Suarez, Real Madrid nayo inadaiwa kumtaka Straika huyo lakini bado haijatoa Ofa rasmi.
Kwa sasa, Suarez, ambae mwenyewe
ameonyesha nia ya kuihama Liverpool lakini anapendelea aende nje ya
England, yupo huko Australia pamoja na Liverpool ambao leo wanacheza
Mechi ya Kirafiki na Klabu ya Melbourne Victory.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :