Mkuu wa jeshi Misri aitisha maandamano
Posted in
No comments
Wednesday, July 24, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
"Ninawasihi watu kuandamana Ijumaa hii kuthibitisha kuwa wananipa mamlaka mimi na jeshi langu kukabiliana na ghasia pamoja na ugaidi,'' alisema Generali Sisi ambaye pia ni waziri wa ulinzi katika serikali mpya.Alikuwa anazungumza katika sherehe za wanafunzi kufuzu chuo kikuu.
Alipinga madai ya migawanyiko jeshini. ''Ninaapa kwa Mungu kuwa jeshi lina msimamo mmoja,'' alisema Sisi.Akigusia hoja ya jeshi kumwondoa mamlakani Morsi, alisema kuwa : '' nilimshauri Morsi kuwa rais wa wamisri wote.''
Na akikumbuka uchaguzi wa urais wa mwaka 2012, wakati Morsi alipochaguliwa, alisema kuwa aliwashauri wanachama wa chama cha Brotherhood kutogombea uchaguzi huo, lakini wakampuuza.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :