RAIS KIKWETE AKABIDHI NYUMBA 8 KWA WAHANGA WA MAPOROMOKO SAME

Posted in
No comments
Thursday, July 11, 2013 By danielmjema.blogspot.com

Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete, ametekeleza ahadi yake aliyoitoa kwa wakazi wa kijiji cha Goha, kata ya Mamba Myamba, Tarafa ya Myamba, wilayani Same Mkoani Kilimanjaro kwa kukabidhi Nyumba nane wahanga wa Maporomoko yaliyotokea mwishoni mwa mwaka 2009.
 
Gama akikagua Nyumba 8 za JK kabla ya kukabidhi kwa wahanga wa Maporomoko yaliyotokea, Novemba 2009 na kuwaacha wakazi 456 wa Kijiji cha Goha bila makazi huku zaidi ya Familia 24 zikiteketea katika Maporomoko Hayo
 
Mkurugenzi wa wilaya ya Same, Joseph Mkude, akitoa taarifa ya ujenzi wa Nyumba hizo 8

Gama akisalimiana na mmoja wa wahanga wa maporomoko ya Same, Eliamini Charles (5), ambaye alipoteza wazazi wake wote katika Maporomoko hayo kabla ya kumkabidhi Nyumba moja kati ya Nyumba 8 za JK.

Gama akizindua nyumba 8 za JK Nyuma yake ni Mkuu wa Wilaya ya Same, Herman Kapufi akimpongeza

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama, katikati ni mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Same, Christopher Irira, na kulia kwake ni Mkurugenzi wa Wilaya Same, Joseph Mkude

Baadhi ya wahanga wa maporomoko ya mwaka 2009 yaliyotokea katika kijiji cha Goha, wilayani Samewakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama aliyewakabidhi Nyumba hizo kwa niaba ya Rais Kikwete
RC-Gama akizungumza na wahanga wa Maporomoko ya Same kabla ya kukabidhi Nyumba 8 ambazo ni sehemu ya ahadi za JK kwa wahanga wa Maporomoko hayo yaliyotokeas mwaka 2009.
Gama akifungua Nyumba kama sehemu ya utekelezaji wa Ahadi ya JK kwa wahanga wa maporomoko, kushoto kwake ni mkuu wa Wilaya ya Same, Herman Kapufi.
Gama akiwa na mkandarasi wa majengo hayo

Mkurugenzi wa Wilaya ya Same Joseph Mkude akitoa maelezo kwa Gama wakati wa makabidhiano ya Nyumba za JK
 
Ahadi hiyo ya Rais Kikwete aliitoa alipotembelea maeneo yaliyothiriwa na Maporomoko ya Ardhi yalitokea kutokana na Mvua kubwa zilizonyesha katika maeneo hayo na Tanzania nzima na kusababisha vifo vya watu 24 huku wengine 45 wakikosa makazi.
 
Akikabidhi nyumba hizo jana kwa niaba ya Rais, Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama amesema kuwa hiyo ni ahadi ya Rais Kikwete, aliyoitoa wakati alipo watembelea wahanga hao, mwishoni Mwa Novemba 2009 na kuahidi kuwajengea nyumba nane wahanga hao wakati alipowatembelea na kuwafariji.

Katika taarifa yake hiyo iliyosomwa na Gama, Rais Kikwete amesema serikali yake inafanya juhudi zote kuhakikisha kuwa wananchi wake wanapata maisha bora ikiwa ni pamoja na makazi bora kwa kila mtu lengo ambalo ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM na moja ya ahadi zake kipindi cha uchguzi.
Aidha amewataka wakazi wa maeneo hayo kuepuka watu wanaojipitisha wakiwalaghai kwa maneno ya kuwalaghai kuwanunulia nyumba hizo na kutoa agizo kwa uongozi wa wilaya kuzisimamia nyumba hizo ili wasiwepo watu wa kubadili umiliki wa nyumba za wahanga hao kwenda kwa umiliki wa watu wengine.


Awali akitoa taarifa fupi amesema katika fedha hizo, ofisi ya waziri Mkuu kitengo cha maafa kilituma shilingi milioni 162, 376,000, huku benki ya NMB ilitoa mchango wa wa saruji mifuko 100 na mabati 400 vyenye thamani ya shilingi milioni 9,757,650.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .