SCHWEINSTEIGER MCHEZAJI BORA UJERUMANI, KOCHA BORA NI JUPP HEYNCKES!

Posted in
No comments
Monday, July 29, 2013 By danielmjema.blogspot.com


Schweinsteiger_wins_German_awardBASTIAN SCHWEINSTEIGER amechaguliwa kuwa ndie MCHEZAJI BORA WA MWAKA 2013 huko Germany baada ya kuwabwaga wenzake wa Timu moja, Bayern Munich, Franck Ribery na Thomas Muller.

Katika Kura iliyoendeshwa na Jarida la Soka maarufu huko Germany, Kicker, na Kura kupigwa na Wanahabari 527 wa Michezo, Schweinsteiger alizoa Kura 92 akifuatiwa na Ribery Kura 87 na Muller 85.

Katika Uchaguzi huo wa Mchezaji Bora, 10 Bora ilitawaliwa na Wachezaji wa Bayern Munich na Borussia Dortmund na Mchezaji pekee wa Klabu nyingine alikuwa ni Stefan Kiessling.
JUPP_HEYNCKESKatika Uchaguzi wa Kocha Bora, Jupp Heynckes, alieiwezesha Bayern Munich Munich kutwaa Trebo Mwezi Mei, yaani Ubingwa wa Germany na Ulaya pamoja na German Cup, aliibuka kidedea kwa kuzoa Kura 383 akimbwaga Kocha wa Freiburg, Christian Streich, aliepata Kura 77.

Schweinsteiger, mwenye Miaka 28, atakabidhiwa Tuzo yake kabla ya Mechi ya ufunguzi ya Msimu mpya wa Bundesliga kati ya Bayern na Borussia Monchengladbach hapo Agosti 9.

Akiongelea kutunukiwa Tuzo hiyo, Schweinsteiger alisema: “Taji hili ni kwa Timu. Imenishangaza kwani kuna wakati vitu vibaya vilizungumzwa dhidi yangu!”

Nae Heynckes alitamka: “Hii ni kilele cha hadithi njema! Ndoto nyingi huwa kweli! ”

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .