KUSITISHWA KWA OPERESHENI WATOA MWANYA WA MAUAJI YA KUTISHA YA TEMBO TANZANIA
Posted in
No comments
Tuesday, December 31, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
Maujia ya tembo yameongezeka
nchini Tanzania tangia serikali ya nchi hiyo kusitisha Opereshieni
tokomeza kutokana na kuwepo madai kwamba kulikuwa na ukiukwaji wa haki
za binadamu.Naibu waziri wa Maliasili na utalii nchini
Tanzania Lazaro Nyarandu amesema kuwa idadi ya tembo 60 wameuawa katika
kipindi cha miezi miwili tu ya mwezi Novemba na Disemba ikilinganishwa
na tembo wawili tu waliouawa mwezi mwa kumi mwaka huu.
Hata hivyo idara za ulinzi zilikubaliana kuwaua majangili watakaobainika wakiwaua tembo hao kipindi ambacho msako huo ulikuwa ukiendelea mwezi Oktoba mwaka huu.Hata hivyo serikali ilisitisha operesheni hiyo kufuatia malalamiko kwamba watekelezaji wa msako huo walikuwa wakikiuka haki za binadamu.

Waziri mkuu wa Tanzania alikaririwa akisema operesheni hiyo ilikuwa na nia njema lakini taarifa za kuwepo vitendo vya mauajia na ukikwaji wa haki za binadamu ndicho ambacho hakikubaliki na serikali.

Hata hivyo matokeo ya uchunguzi wa kamati maalumu kuhusiana na kuwepo kwa ukiukwaji wa haki za binadamu ndiyo uliosababisha Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete kuwafukuza kazi mawaziri ,Shamsi Vuai Nahodha wa jeshi la ulinzi, Emmanuel Nchimbi wa mambo ya ndani,waziri wa Utalii na maliasili Khamis Kagasheki na waziri wa Maendeleo ya Mifugo David Mathayo.

Nchi za kutoka bara la Asia ndizo zinazodaiwa kujihusisha Zaidi na biashara ya pembe za ndovu hali inayoongeza kasi ya ujangili na mauaji ya tembo nchini Tanzania
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako


0 MAOINI :