BREAKING NEWZZZZZZZ: STOO YA CCP YAWAKA MOTO
Posted in
Matukio
No comments
Wednesday, February 12, 2014
By
danielmjema.blogspot.com
TAARIFA
zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa, Stoo ya kuhifadhia vifaa vya maaskari
katika chuo cha mafunzo ya polisi Moshi
(MPA) maarufu kama CCP, imewaka moto.
Kwa mujibu
wa taarifa hizo zilizothibitishwa na Mkuu wa Chuo hicho, CP-Matanga Mbushi,
moto huo ulianza majira ya saa 3:45 alasiri.
Akizungumza
na Kijiwe chetu Blog, Kamanda Matanga Mbushi amesema kuwa chanzo cha moto huo
haujabainika japo moto huo unaonekana kuanzia katika Nguzo ya Umeme ulioko
jirani na jengo la stoo.
Amesema
maaskari wake walishirikiana kuuzima moto huo na kuokoa vifaa vingi na kwamba
kinachoendelea kwa sasa ni zoezi la kufanya tathmini ambapo taarifa kamili
zitatolewa baadae.
Kamanda
huyo anatarajia kukutana na waandishi wa Habari Kesho asubuhi ambapo taarifa
kamili ya chanzo na athari ya moto huo itatolewa.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :