WAMILIKI WA MABASI MADOGO WAGOMA KUTOA HUDUMA KWA MASAA 9 MJINI MOSHI.

Posted in
No comments
Monday, March 24, 2014 By danielmjema.blogspot.com

Kituo kikuu cha mabasi yaendayo sehemu mbalimbali ndani ya mkoa wa Kilimanjaro na Arusha ikiwa haina gari baada ya wamiliki wa magari yaendyo maeneo hayo kugoma kutoa huduma.
Kutokana na mgomo huo ndipo madereva wa magari hayo na makondakta wakaamua kugeuza stendi hiyo uwanja wa mpira wa miguu likapigwa mbungi kati ya madereva na makondakta.
Ndipo askari walipoamua kuingilia kati na kuzuia mchezo huo uliokuwa hauna waamuzi wala milingoti ya kufunga magoli.
Ulinzi ukaimarishwa zaidi.
Baadhi ya makondakta na madereva wa magari hayo wakatiwa mikononi.
Hata hivyo hatua ya kukamatwa kwa madereva na makundakta kiliwatia hasira wapiga debe wakaamua kulipopoa gari la polisi kwa mawe na kuvunja kioo cha nyuma kama inavyoonekana hapa.
Abiria walilazimika kupanda gari la kusafirisha magazeti ya Mtanzania.

Mwandishi Wetu, Moshi

MAGARI yanayofanya safari zake katika Barabara ya Moshi-Arusha zimegoma kufanya safari kwa takribani masaa 9 yakipinga kulipishwa bondi ya makosa ya shilingi elfu 30 katika kila kituo kwa kosa lilelile.

Wakizungumzia chanzo cha mgomo huo, baadhi ya wamiliki na madereva wa magari yaendayo, Marangu, Rombo, Arusha, Rau pamoja na magari yote yanayotoa huduma katika maeneo ya mijini kama vile pasua KCMC na Uru, wamesema sababu ya msingi ya kufanya mgomo huo kulishinikiza kitengo cha usalama barabarani na Mamlaka ya usafiri wa majii ya nchi kavu (SUMATRA), kuangalia upya tozo hizo.

Akizungumza kwa niaba ya madereva hao, katika kikao kilichoitishwa na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,  Leonidas Gama, na kukutanisha pande zote kwa maana ya Akiboa, Jeshi la Polisi na SUMATRA, Mwenbyekiti wa Akiboa kanda ya Kaskazini, Hussein Mrindoko, amesema kiini cha mgomo huo ni kitendo cha udhalilishaji wanaofanyiwa na askari wa usalama barabarani.

Kwa upande wake Mkuu wa kituo kidogo cha polisi Moshi mjini OCS, Hendry Nguvumali anayelalamikiwa kulazimisha faini kinyume cha sheria, pamoja na kufanya kazi akiwa mlevi amesema malalamiko yote yametokana na ukweli kwamba anafanya kazi kwa mujibu wa sheria za Jeshi la polisi.

Akijibu malalamiko yaliyolekezwa kwa SUMATRA kuhusu ucheleweshaji wa stika na ukamataji wa leseni za biashara ya usafiri, Meneja wa mamlaka hiyo mkoa Kilimanjaro Fabian Nyang’oro amesema SUMATRA imekuwa ikitekeleza majukumu yake kwa mujibu wa taratibu na sheria za usalama barabarani pamoja na sheria ya umiliki wa vyombo vya usafiri.

Amesema endapo mmiliki wa Chombo cha biashara  ya usafiri atakiuka sheria hizo wao kama wasimamizi kazi yao sio kukamata magari bali kuhakikisha stika ambazo zimechukuliwa kinyume cha taratibu wa utoaji wa leseni za biashara zinafutwa.

Naye Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama, alisema kimsingi tatizo hilo halikutakiwa kuwepo maana taratibu zote za kisheria ziko wazi ambapo aliitaka SUMATRA kama wenye dhamana kuu na usafiri barabarani kuhakikisha wanakaa meza moja na Jeshi la Polisi pamoja na Akiboa kuzungumzia malalamiko yote yaliyowasilishwa na kuyapatia ufumbuzi.

Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi mkoani hapo, Robert Boaz, aliwataka Madereva kufuata sheria na kuwataka kuacha kulalamika ambayo kimsingi wanayasababisha wao kutokana na kukiuka taratibu za usalama barabarani.

Amesema baada ya kutolewa kwa taarifa ya Mkoa wa Kilimanjaro kuwa ya pili kwa ajali za barabarani, Jehsi la Plisi mkoani hapo lilichukua hatua ya kuhakikisha inakabiliana na tatizo hilo ambalo alisema kwa asilimia kubwa husababishwa na uzembe wa madereva wawapo barabarani.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .