JARIBIO LA KUTEKA NYARA MTOTO WA MWANAHABARI LASHINDIKANA
Posted in
Matukio
No comments
Friday, May 2, 2014
By
danielmjema.blogspot.com
Rehema Matowo-mwandishi wa Mwananchi Kilimanjaro |
Na Mwandishi Wetu, Moshi
Kamanda wa Polisi mkoa Kilimanjaro, Robert Boaz amewatahadharisha wazazi wenye
watoto wadogo, kuwaelimisha wafanyakazi wa ndani kutowakabidhi watoto wao kwa
watu wasiowajua.
Tahadhari
hiyo inafuatia tukio la jana saa 7:00 mchana ambapo watu watatu wakiwa na
pikipiki mbili, walifanya jaribio la kutaka kumteka mtoto wa mwandishi wa gazeti
hili mkoa Kilimanjaro, Rehema Matowo.
Watu
hao walifika nyumbani kwa mwandishi huyo saa 7:00 mchana na kumweleza mfanyakazi
wa ndani kuwa wametumwa na baba mzazi wa mtoto huyo ili wamchukue kutoka Soweto
na kumpelekea katikati ya mji.
“Aliwauliza
mbona baba wala mama hajapiga simu?… hao watu wakasisitiza wametumwa kumchukua
mtoto huyo tena wakimtaja kwa jina mtoto na jina la baba”alisema Rehema. Mtoto
huyo ana umri wa miaka miwili na miezi nane.
Hata
hivyo mfanyakazi huyo aliwatilia mashaka watu hao na kurudi ndani kisha kufunga
geti la nyumba hiyo lakini watu hao wakagonga geti hilo mara kadhaa wakisisitiza
kupewa mtoto.
Wakati
watu hao wakiendelea kugonga geti hilo, mfanyakazi huyo alimpigia simu mwandishi
huyo na kumweleza ambapo alimtahadharisha kutofungua geti hilo kwa vile ni jambo
la ajabu.
“Tumeondoka
na mume wangu asubuhi kwenda ofisini na kila mmoja anafanya kazi ofisi tofauti
na isingewezekana kumhitaji mtoto bila mimi kunijulisha na nilipomweleza naye
alishtuka sana”alisema.
Kutokana
na tukio hilo, Kamanda Boaz aliwatahadharisha wazazi kuwa makini ikiwamo kuwapa
elimu wafanyakazi wao ili kuchukua tahadhari pindi wanapokutana na matukio
yasiyo ya kawaida.
“Huwezi
kujua dhamira yao hasa ilikuwa ni nini, inawezekana walitaka kumteka nyara mtoto
au kwa madhumuni mengine maana hivi sasa kuna matukio ya ajabu ajabu huwa
yanaibuka,”alisema.
Kamanda
Boaz, aliwataka wananchi kuchukua tahadhari pale wanapowaona watu wakiwa katika
harakati zinazotilia shaka hasa katika maeneo yao na watoe taarifa polisi mara
moja.
Vitendo
vya utekaji nyara watoto mkoani kilimanjaro viliwahi kutikisa mkoa huo
miaka miwili iliyopita ambapo watoto walikuwa wakitekwa nyara na
kupelekwa katika mji wa Busia nchini Uganda na baadae kurudishwa baada
ya wazazi kulipa fedha kwa watekaji kupitia Benki ya Stanbic
Source:Mwananchi
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :