UHOLANZI DHIDI YA ARGENTINA NI MECHI YA KUONESHANA UMWAMBA; NANI ATAINGIA FAINALI?

Posted in
No comments
Tuesday, July 8, 2014 By danielmjema.blogspot.com


Netherlands vs. Argentina: Updated Form Analysis for 2014 World Cup Semi-Final

Argentina na Uholanzi wanakutana kesho katika mchezo wa nusu fainali ya Pili ya kombe la dunia mwaka 2014 itakayopigwa katika uwanja wa Arena Corinthians, mjini Sao Paulo, huku swali kubwa likiwa ni nani ataibuka mbabe katika mpambano huu ambao wengi wanautafsiri kama mechi ya kuoneshana umwamba?

Wakiwa wamefanikiwa kuwafunga Ubegiji na Costa Rica katika Robo fainali, lakini hamna ushindi hata mmoja kati ya timu hizi ni ya kuridhisha kwani wakati wadachi wakisubiri ushindi wa matuta, wenzao Argentina baada ya kupelekwa puta na Ublgiji waliambulia goli moja tu lililofungwa na Gonzalo Higuain.

Hata hivyo, haimaanishi kwamba mchezo kati ya timu hizi mbili haitakuwa ya kuvutia ukizingatia ukweli kwamba Argentina na uholanzi wote wana kiu ya kutwaa Kombe hili katika ardhi ya bingwa mara tano, Brazil.
 

Uholanzi wanaonekana Bora
 
Ukizitizama nchi hizi, kwa maana ya timu ya Argentina na Uholanzi utabaini kuwa, Jeshi la Luis Van Gaal wana nafasi kubwa ya kutinga hatua ya Fainali na kuwaondosha Argentina ambao wanaonekana kutegemea uwezo wa mchezaji mmoja, hapa nawazungumzia, Lionel Messi, Angel Di Maria, ambaye atakosekana katika huu mchezo na Gonzalo Higuain.

Ubora wa Uholanzi ulianza kudhihirika baada ya kuwakandamiza Bingwa watetezi, Uhispania goli 5-1, kabla ya kutoka sare ya 0-0 na timu ngumu ya Costa Rica, wakiinyuka Australia 3-0, Chile wakila 2-0 na magoli ya mwisho mwisho waliopata katika hatua ya 16 bora dhidi ya Mexico na kubadili mchezo yanatosha kukuonesha kuwa Vijana hawa wameamua mwaka huu.

 
Lakini katika kuhakikisha kuwa kikosi hiki kiko vizuri zaidi ya kikosi cha Alejandro Sabela, kila goli lililofungwa na Uholanzi yalitoka kwa wachezaji mbalimbali (Arjen Robben, Memphis Depay na Robin van Persie) na sio mchezaji mmoja (Lionel Messi magoli 4 kati 8 walizofunga).
 

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .