SKYLIGHT BAND YAKWEA PIPA KUTUMBUIZA OMAN, YAWAOMBA RADHI MASHABIKI WAKE DAR

Posted in
No comments
Friday, October 3, 2014 By danielmjema.blogspot.com

10494817_372473116244006_3617867818539775125_n

Uongozi wa Skylight Band unawaomba radhi mashabiki wake wa Dar es Salaam kwa kutokuwepo nchini kwa ajili ya kutoa burudani jioni ya leo kwenye uwanja wao wa nyumbani Thai Village Masaki pamoja na siku ya Jumapili kwenye Skylight Sunday Bonanza katika kiota cha maraha Escape One kutokana na kupata mwaliko wa kutumbuiza nchini Oman.

Skylight Band watarejea nyumbani wiki ijayo na kuendelea na ratiba zao kama kawaida ambapo siku ya Ijumaa tarehe 10/10/2014 watakuwepo Thai Village pamoja na Jumapili tarehe 12/10/2014 kwenye Skylight Sunday Bonanza ndani ya kiota cha maraha Escape One.

Skylight Band inarudia tena kuwaomba radhi mashabiki wake wa Dar na kuendelea kuwashukuru kwa sapoti wanayoipata na inawapenda sana.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .