ARUSHA: RAIS UHURU KENYATTA WA KENYA NA RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI WA TANZANIA WAWAONGOZA WAKUU WA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI (EAC) KUSHIRIKI KATIKA UZINDUZI WA BARABARA YA ARUSHA-HOLILI/TAVETA-VOI KM 234.3

No comments
Thursday, March 3, 2016 By danielmjema.blogspot.com

Rais wa Tanzania John Magufuli na mwenzake wa Kenya Uhuru Kenyatta wanaweka jiwe la msingi katika barabara itakayounganisha mji wa Arusha nchini Tanzania na mji wa Voi nchini Kenya. Barabara hiyo kutoka Arusha hadi Taveta inatarajiwa kurahisisha uchukuzi na kuimarisha biashara kati ya mataifa hayo mawili. Ina umbali wa kilomita 234 na ni sehemu ya mradi mkubwa wa barabara inayotoka Arusha na kupitia Holili na Taveta hadi Mwatate. Jiwe la msingi limewekwa na marais hao wawili eneo la Tengeru, Arusha.


Matukio katika picha:


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kabla ya uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kabla ya uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta akizungumza jambo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  kabla ya uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais wa Uganda Yoweri Museveni  kabla ya uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama pamoja na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, Uganda, Yoweri Meseveni na Rais wa Zanzibar Ali Mohamed Shein wakati Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ukipigwa kabla ya uzinduzi wa barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wananchi wa Arusha hawapo pichani kabla ya ya uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Rais Uhuru Kenyatta, wakiwaongoza Marais wa Uganda, Makamu wa Rais wa Sudani Kusini pamoja na Burundi kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa mitambo itakayotumika katika ujenzi wa barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimwagilia mti maji pamoja na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (Nairobi) Gabriel Negata mara baada ya uzinduzi wa barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.


Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya Nchi. (PICHA NA IKULU YA TANZANIA)

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .