PREZZO AANIKA 'HIV STATUS' YAKE INSTAGRAM

Posted in
No comments
Saturday, March 19, 2016 By danielmjema.blogspot.com


KUFUATIA uvumi wa muda mrefu kwamba, Rapa Prezzo, raia wa Kenya ameathirika na virusi vya gonjwa hatari la Ukimwi, hatimaye msanii huyo ameibuka na kuvunja ukimya kwa kuanika 'Status' yake.

Uvumi kuhusu kuathirika kwa Prezzo zilianza kusambaa katika mitandao ya kijamii, kutokana na kitendo cha msanii huyo kupoteza uzito kwa kasi katika siku za hivi karibuni, ambapo wengi wamekuwa wakisema kuwa, gwiji huyo anayetambulika kwa sifa ya kuwa 'Cassanova' ameukwa!

Rapa huyo wa Mafans alilazimika kuingia hospitali kwa ajili ya kufanya vipimo na baada ya kuridhika na matokeo, alisambaza matokeo ya Status yake kwa lengo la kuvunjwa ukimya na kuthibisha kile kinachosemwa juu yake.

Prezzo alitupia ripoti hii ya vipimo vyake katika mtandao wake wa Instagram ambapo aliambtanisha na maneno haya  “Know ur status, I just had to coz some of y’all talk too much #GodsSon #Alhamudulillah #Rapcellency (sic).”

Source: https//:www.cizentv.co.ke

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .